• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Serikali Kuwakamata Wasiodai na Wasiotoa Risiti za Biashara

Imetumwa: February 17th, 2021

Mkuu wa wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ameagiza Kamati ya ulinzi na usalama kuhakikisha inashirikiana na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kuwakamata wafanyabiashara na wateja wanaouza na kununua bidhaa bila kutoa na kudai Risiti za malipo.

Sabaya amesema kuwa watu hao wamekuwa wakisababisha Serikali kukosa mapato stahiki na mamlaka zinazokusanya mapato kushindwa kufikia malengo ya ukusanyaji kodi na maduhuli ya serikali.

Lengai Ole Sabaya ametoa maagizo hayo wakati wa kikao maalum na watendaji wa TRA, Maafisa biashara wa halmashauri pamoja na watendaji wanaohusika na masuala ya fedha wote kwa pamoja wamejadili kuhusu kupandisha mapato ya wilaya ya Hai katika mwaka wa fedha 20021/22.

Sabaya ameagiza hayo baada ya kubainika kuwa baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu kukwepa kulipa kodi na kushindwa kutoa risiti kwa wateja na kuikosesha serikali mapato na kusababisha mamlaka za serikali kushindwa kufikia malengo ya ukusanyaji wa kodi. 

“Naagiza kuanzia Sasa OCD na timu yako kwa kushirikiana na TRA na halmashauri fanyeni operation ya kuwakamata wanaofanya biashara na kushindwa kutoa na kupokea risiti maana ndiyo wanaoikosesha serikali mapato”. Ameagiza Sabaya.

 “Utakuta Mtu ananunua mzigo wa mamilioni ya fedha hadai risiti au anafanyia ujanja ujanja wa kupata risiti iliyoambatana na biashara iliyofanyika kamateni weka ndani tupate mapato tujenge barabara, shule, hospitali, tununue dawa na kuleta maendeleo kwa wananchi “Amesema Mkuu wa wilaya Sabaya

Hata hivyo Sabaya ameeleza kwamba hakuna duka lolote lillilofungwa na Mamlaka ya mapato TRA wala akaunti za wafanyabiashara bali wafanya biashara wenyewe wamekuwa wakitoa bidhaa nje ya maduka na kuwapa wafanyabiashara wadogo (machinga) wakauze nje na baadaye kumletea faida na kupewa posho yao ya siku hivyo kusababisha TRA kukosa mapato.

Pamoja na hayo Sabaya amabaini mbinu nyingine inayotumiwa na wafanyabiashara kukwepa kodi za serikali kwa kuuza bidhaa zao kwa mtindo wa kuwakopesha wateja wao na kupokea malipo kwa awamu bila kutoa risiti; mtindo aliouita ‘black market’ na kuziagiza mamlaka husika kufuatilia na kuwakamata watu wanaotumia mtindo huo ili kutambua kama wanalipa kodi stahiki au la.

Naye Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Mapato (TRA) wilayani Hai, Ester Martin Mallya amesema  wamekusudia kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 4.6 kwa mwaka wa fedha wa 2020,2021 huku akibainisha kuwa iwapo kutafanyika ufuatiliaji wa kina nakuziba mianya wa kukwepa kodi basi mamlaka hiyo inaweza kukusanya zaidi ya malengo waliyojiwekea.

Amesema katika ukusanyaji wa mapato wanakutana na vikwazo vya wafanya biashara kuuza bidhaa na kuacha kutoa risiti au wakitoa wanatoa ya pesa ndogo jambo ambalo amemuomba mkuu wa wilaya kulisimamia kwa nguvu zote waweze kufikia malengo ya ukusanyaji.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyabiashara wa wilaya Hai; Mwenyekiti wa wafanyabiashara eneo la stand ya Bomang’ombe Anderson Soni ameshukuru kikao cha pamoja na Mamlaka ya Mapato (TRA) na kupata mafunzo kwani wamekua wakiogopa kukutana nao na kufanya mashairiano ya juu ya kiendesha biashara.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai