Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Hai Trael Mboya amewataka wananchi kushiriki kikamilifu miradi mbalimbali inayotekelezwa katika maeneo yao ili iweze kuwanufaisha.
Amebainisha hayo wakati wa ziara ya Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ikikagua Ujenzi wa madrasa 3 na matundu 6 ya vyoo Katika Shule ya Msingi Tolu vilivyo garimu shilingi 88,600,000.
Mboya amesema kuwa endapo wananchi watashirikishwa ipasavyo katika miradi iliyoko katika maeneo yao ,wataitunza vyema kwani watatambua mchango wao katika miradi hiyo.
Hata hivyo Mboya amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi Katika Wilaya ya Hai na Mhe.Mbunge wa Jimbo la Hai Saashisha Mafue kwa kuomba na kufatilia maombi mbalimbali ya Miradi inayo ombwa Katika ngazi mbalimbali.
Naye Diwani wa kata ya Romu Wilaya ya Hai Salim Mfoi amewapongeza wananchi kwa jinsi ambavyo walijitoa kwa ajili ya kuchimba mashimo ya vyoo pamoja na kuchimba msingi wa madarasa matatu katika shule ya msingi Tolu iliyoko katika kata ya Romu.
Kitongoji cha Bomani
Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai
Simu: 0754553560
Simu ya Mkononi: 0754553560
Barua Pepe: ded@haidc.go.tz
Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai