• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Maliasili Washauriwa Kuboresha Fidia Madhara Yanayosababishwa na Wanyamapori

Imetumwa: May 12th, 2021

Katibu Tawala Wilaya ya Hai Upendo Wella ameiomba Wizara ya Maliasili na Utalii kuangalia viwango wanavyopatiwa wahanga wa matukio ya ajali zinazohusisha wananchi na wanyama pori.


Ameishauri Wizara hiyo kuangalia namna ya kuboresha kiwango kwa kuzingatia hali halisi ya maisha pamoja na thamani ya uharibifu au madhara yaliyotokea.


Wella ametoa ombi hilo kwa Wizara wakati akishuhudia makabidhiano ya fedha za kifuta jasho na kifuta machozi kwa wananchi 4 wa Wilaya ya Hai ambao wamepata madhara na hasara vilivyosababishwa na wanyama pori.


Akiongoza wataalamu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Afisa Wanyamapori Mkuu Nassoro Wawa amesema wamekuja kuwapa sehemu ya fidia wananchi 2 ambao wengine wamepata majeraha yasiyo ya kudumu na wengine 2 ambao mazao yao yaliharibiwa na wanyama.


Wawa amesema kanuni zinaelekeza kutoa kifuta machozi kwa wananchi ambao wamepata majeraha ambapo shilingi 200,000 hutolewa kwa aliyepata majeraha yasiyo ya kudumu na shilingi 500,000 kwa majeraha au kilema cha kudumu huku wakitoa kifuta jasho cha shilingi 100,000 ekari kwa wale ambao mazao yao yameharibiwa na wanyama pori na shilingi 1,000,000 kwa mwananchi aliyeuwawa na wanyama.


Aidha Afisa Wanyamapori anayehudumu katika Wilaya za Hai na Siha Lyimo amesema matukio ya wanyamapori kujeruhi au kuharibu mazao yanatokana na wananchi kufanya shughuli za kilimo kwenye maeneo ya mapito ya wanyama pori au wanyama kutafuta malisho hasa wakati wa kiangazi huku akisisitiza kuwa fidia inalipwa kwa wananchi waliothibitikshwa kuwa nje ya maeneo ya hifadhi za wanyama pori.


Kwa upande wake Charles Palanjo mkulima wa Kijiji cha Sanya Station ambaye sehemu ya shamba lake liliharibiwa na mnyama wa porini (nyati) ameishukuru Serikali na maafisa maliasili wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai kwa ushirikiano waliompa hadi na kumwelimisha taratibu za kufuata hadi kufikia kulipwa kifuta jasho.


Amewaasa wananchi wengine kuacha kulalamika wanapokutana na uharibifu bali wawasiliane na mamlaka husika ngazi ya wilaya kwa ajili ya kutoa taarifa ili taratibu za kisheria zifuatwe.


Serikali imeendelea kusisitiza kufuata taratibu hasa wananchi kuweka makazi na kufanya shughuli za maendeleo mbali na maeneo ya wanyamapori ili kuepusha madhara lakini pia kuwahimiza wananchi wote kuwa sehemu ya kuhifadhi na kulinda maliasili zilizopo kwa manufaa ya Taifa.






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai