• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Taarifa Idara ya Kilimo

TAARIFA YA IDARA YA KILIMO UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

  • MRADI WA TANSHEP
  • Katika msimu wa 2018/2019 Halmashauri  ya wilaya inatekeleza mradi wa TANSHEP (Tanzania Smallholder Horticultural Empowerment Promotion) unaofanyika kwa ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Japan (JAICA) unaoendeshwa katika wilaya 2 za Mkoa wa Kilimanjaro ikiwemo wilaya yetu ya Hai. Lengo la mradi huu ni kuhamasisha na kuwawezesha wakulima wadogo wadogo wa mbogamboga kubadili fikra kutoka kilimo cha kawaida kuwa kilimo biashara ambacho huanza na utafiti wa masoko kisha kuzalisha kulingana na mahitaji ya soko. Mradi huu una kauli mbiu isemayo ANZIA SOKONI MALIZIA SHAMBANI KWA KIPATO ZAIDI. Mradi umefadhili vikundi 11 vinavyolima mbogamboga kwa kutoa mafunzo ya namna ya kupata masoko ya mazao kabla ya kuanza shughuli za Kilimo.

Ni mradi unatumia mtazamo wa shep katika kilimo cha Tanzania na mwishowe kutengeneza mtazamo unaoendana na mazingira halisi ya Tanzania. Shep ilianzia Japani  na kwa bara la Africa ulijaribiwa Kenya 2006 ambako wakulima wadogowadogo wa Kenya walikuwa na chanagamoto nyingi na tayari wamepata ufumbuzi wa changamoto hizo ambapo kipato kimeongezeka, ujuzi na maarifa katika kulima vimeongezeka, kalenda ya kupanda na kuvuna inafuatwa na mabadiliko katika matumizi ya pembejeo. Mradi huu kwa sasa umesambaa katika nchi 10 za bara la Africa.

Mradi huu ni wa miaka mitano kuanzia Julai 2019 hadi Julai 2023. Katika kanda ya kaskazini mradi huu unatekelezwa katika mikoa ya Tanga wilaya ya Lushoto na Bumbuli, Kwa Kilimanjaro Hai na Moshi na Arusha wilaya za Meru na Karatu.

Kwa ngazi ya wilaya mradi umeanza Julay 2019 ambapo vikundi vilivyochaguliwa kutekeleza mradi ni kumi na moja (11) navyo ni Shamiri toka Kijiji cha Kawaya, Neema Envirocare cha Nshara, Umoja cha Mkombozi, Leira kijiji cha Rundugai, Tupendane kijiji cha Mkalama, Upendo na Amani vya kikavu chini, Orori kilimo kwanza na mwamko vya kijiji cha Orori, Wamboma cha shirinjoro na Mshikamano cha Kimashuku.

Usimamizi wa utekelezaji wa mradi huu unafanyika kwa ushirikianovwa wawakilishi wa JICA, Tamisemi, Wizara ya kilimo,  Ofisi ya mkuu wa mkoa na na wawezeshaji sita wa ngazi ya wilaya.

Matokeo makubwa yanayotarajiwa kwa wakulima baada ya mradi kukamilika ni kama ifuatavyo;-

Kuwawezesha wakulima kulima kwa tija kwa kuwaunganisha na wadau mbalimbali ka ma taasisi za fedha na wauza pembejeo.

Kuwawezesha wakulima kuwa huru na kujiamini katika kulima na kuuza mazao yao.

Kujifunza kwa wakulima wengine na kuungana katika kuzalisha na kuuza ili waweze kutoka kwenye kulima na kuuza na kuelekea kwenye kilimo biashara kwa maana yakulima kwa ajili ya kuuza.

Wakulima watawezeshwa kumiliki kile wanachokifanya  pia kuwa na mahusiano na wadau mbalimbali kwenye mnyororo wa thamani ili kujifunza kutoka kwao pamoja na kupata maarifa mapya.

2. KOROSHO

Zao la Korosho ni zao jipya kwa wilaya ya hai. Katika msimu wa Kilimo 2017/2018,  Halmashauri ilipokea toka Bodi ya Korosho Tanzania jumla ya kilo 45 za mbegu za Korosho, kilo 25 za viriba (sheets), kilo 22  za matandazo, mwongozo na nakala ya mkataba wa kuzalisha miche. Kwa kuzingatia mwongozo, halmashauri iliteua Kikundi cha Mawoi Enviromental Care kusaini mkataba wa uzalishaji miche.

Uzalishaji na usambazaji wa miche 

Kikundi hiki kilisaini mkataba wa kuzalisha miche 6,300 lakini kiliweza jumla ya miche 5,919 iliyosambazwa kwa wakulima. Kutokana na mwitikio na hamasa kubwa iliyokuwepo miongozni mwa wakulima , halmashauri iliweza kupata miche  mingine 1,000 kutoka jeshi la Magereza - Karanga na kufanya idadi ya miche iliyosambazwa kwa wakulima kufikia  6,919. Halmashauri inakusudia kuzalisha na kusambaza angalau miche 10,500 kwa mwaka ambapo inahitaji jumla ya kilo 75 za mbegu za zao la Korosho kwa msimu wa 2020/2021 ili kuendeleza zao la Korosho.

Mafanikio

  • Kuhamasisha wakulima hasa wa ukanda wa kati na tambarare kulima zao la Korosho
  • Kuzalisha miche yenye ubora bila hata kupata mafunzo mahususi ya Kilimo cha Korosho licha ya kuwepo kwa changamoto ya mvua kubwa na magonjwa mengi
  • Kusambaza miche yote kwa wakulima takribani 327 ndani ya Wilaya pamoja na kutokuwa na bajeti toka bodi ya Korosho kwa ajili ya kutekeleza shughuli hizi

 

Changamoto

Pamoja na wakulima kuhamasika kulima zao la Korosho, kuna changamoto zinazowakabili kama ifuatavyo;-

  • Wataalamu, wazalisha miche, wakulima na viongozi mablimbali kutopata elimu rejea ya zao la Korosho ili kuwa na uelewa kwa undani
  • Kutokuwa na vitendea kazi kama usafiri na shajala
  • VANILLA

Kilimo cha Vanilla Wilaya ya Hai kilianza mwaka 2000 kutokana na mafunzo yaliyotolewa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu Cha Sokoine Morogoro, lakini kutokana na kuyumba kwa soko la Vanilla, uzalishaji wake uliendelea kufifia hadi mwaka 2011 ambapo soko lake lilianza kuimarika na kufanya wakulima waanze tena Kilimo hicho. Wakulima walipata mafunzo ya uzalishaji kutoka Shirika la Msalaba Mwekundu kupitia mashamba darasa 8. Pamoja na mafunzo hayo, Shirika hilo pia limewajengea wakulima kiwanda cha kusindika Vanilla pamoja na vituo 4 vya kukusanyia Vanilla katika vijiji vya Mudio, Nkwansira, Uswaa/Mamba na Kyuu. Pia Kampuni ya Natural Extract Industries (NEI) imekuwa ikitoa mafunzo ya uzalishaji, ukarabati wa mfereji, marando ya ruzuku na kuwaunganishia baadhi ya wakulima miundo mbinu ya umwagiliaji. Kwa sasa jumla ya wakulima takribani 1,535 wa wilaya ya Hai wanajihusisha na Kilimo hiki ambapo wanaendelea kupanua mashamba yao kila mwaka. Hadi sasa jumla ya miche takribani 22,810 ya Vanilla imeoteshwa sawa na hekta 34, uzalishaji wa sasa kwa mwaka ni Tani 1.4.

Halmashauri kupitia Idara ya Kilimo imeandaa andiko la mradi wa kuendeleza zao la vanilla ambapo ilipata TZS 16,000,000.00 kutoka benki ya NMB Kanda ya Kaskazini. Uhamasishaji ulioambatana na mafunzo ya Kilimo cha Vanilla umeshafanyika kwenye Kata 10 zenye jumla ya vijiji 43 ambapo lengo lilikuwa ni kutoa mafunzo kwa wakulima 30 kwenye kila Kijiji sawa na jumla ya wakulima 1,290.

 

Mwitikio wa wakulima umekuwa ni wa kuridhisha kwa baadhi ya maeneo na kwa sasa wanaandaa mashimo ya kuotesha Vanilla ambapo wanatarajiwa kupata miche ya Vanilla isiyopungua kwa bei ya ruzuku ya TZS 1,000 kwa mche. Ununuzi wa miche  unafanyika kwa awamu ambapo kwa awamu ya kwanza jumla ya miche 2,800 yenye thamani ya TZS 7,000,000.00 imenunuliwa kutoka kikundi cha  Mauki Vanilla Group na inatarajiwa kusambazwa kwa wakulima. Lengo kuu ni kununua na kusambaza miche 8,200 yenye thamani ya TZS 20,500,000.00, hii itawezekana kutokana na kutumia mfumo wa kusambaza miche kwa wakulima kwa bei ya ruzuku ya TZS 1,000 kwa mche. Aidha, Kikundi cha Mauki wanaendelea kuzalisha miche mingine ili iweze kununuliwa na kusambazwa kwa wakulima wakati wa msimu wa mvua za vuli.

  • ZAHANATI YA AFYA YA MIMEA

Halmashuri imekuwa ikitoa mafunzo ya namna ya kudhibiti visumbufu vya mimea kupitia zahanati ya afya ya mimea. Wataalamu wa Idara ya kilimo kitengo cha mazao walipata mafunzo kutoka kwa madaktari wa mimea (Plant Doctors) kutoka Shirika la CABI international mwaka 2011 lenye makao makuu Uingereza. Wataalamu wamekuwa wakitoa elimu ya matumizi sahihi ya viuatilifu katika kudhibiti visumbufu kwenye mimea kwa kutambua madaraja ya sumu wakati wa matumizi kwa kuangalia rangi ya kidandiko cha sumu (Rangi nyekundu, Njano, bluu na Kijani) eneo lenye picha ya namna ya kujikinga wakati wa matumizi ya sumu husika. Lengo kuu ni kudhibiti madhara ya sumu iliyotumika kwenye mazao kumfikia mlaji.

Huduma za Zahanati ilikuwa inatolewa Siku za soko hasa soko la Mula, Kwasadala , Hai mjini na Rundugai, lakini kwa sasa huduma hii imesimama kwa kuwa wataalamu waliopata mafunzo ya namna ya kuendesha zahanati ya afya ya mimea kustaafu. Hivyo kwa sasa huduma hii imekuwa ikitolewa kwenye mashindano ya maonesho ya wakulima nane nane ambayo hufanyika Arusha kila mwaka kuanzia tarehe 1.08.2020 hadi 10.08.2020

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai