• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Fursa za Uwekezaji


FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA WILAYA  YA HAI

  1. Eneo la uwekezaji (EPZ – Export Processing Zone):  Wilaya imetenga eneo kubwa la 463 Ha.kwa ajili ya ujenzi wa ukanda wa viwanda vya kuzalisha mali za kusafirisha nje ya nchi (EPZ – Export Processing Zone),  eneo hili lipo katika barabara kuu inayoelekea Arusha.
  1. Eneo la Machine Tools: -  Eneo hili lenye viwanja vyenye jumla ya hekta 430 lilikuwa linatumika awali katika uzalishaji wa spare za magari na viwanda, hata hivyo hivi sasa limewekwa wazi kwa ajili ya uwekezaji wa bidhaa za viwandani.
  1. Kituo cha uzalishaji umeme: - Kikuletwa Power Station  -  Kituo hiki kilitumika katika kuzalisha umeme katika enzi za Mkoloni, hata hivyo pamoja na mitambo yake kuharibika, bado kuna mazingira mazuri ya maji ya kutosha ambayo yanaweza kuzalisha kiasi cha Watts 6 kwa siku na kuuzwa kwenye Grid ya Taifa na hivyo kupunguza tatizo la Kitaifa la umeme lilipo.
  1. Eneo la Utalii:  - Wilaya ya ina vivutio muhimu vya utalii hii ni pamoja na Chemichemi ya Chekimaji inatoa maji ya moto pamoja na Mlima Kilimanjaro.  Vivutio hivi vinaweza kutumika katika ajira kwa vijana (ajira kwa wapanda mlima).
  1. Wilaya ina uwezekano kuwekeza katika Kilimo cha Umwagiliaji:  kwa kujenga mabwawa na mifereji ya umwagiliaji:

Fursa nyingine ni uwekezaji katika shughuli za ufugaji ambapo vyama vya ushirika vinaweza kuanzisha mashamba ya ufugaji wa kisasa.

Uwekezaji katika kilimo cha maua

  1. Uwekezaji katika utalii:

Yako maeneo ya kutosha kwa ajili ya uwekezaji wa Hoteli za Kitalii hasa ukizingatia ni eneo lililo karibu na uwanja wa ndege wa Kimataifa (KIA).

Kuwekeza katika vivutio vya Kitalii

Aidha upo uwezekano mkubwa wa kuwekeza katika uhigadhi wa masuala ya kihistoria (makumbushio ya kihistoria).

  1. Uwekezaji katika elimu:

Kuna fursa ya uwekezaji katika shule za ufundi na pia uwekezaji katika vyuo na vyuo vikuu.

Uwekezaji katika viwanja vya michezo na ujenzi wa vyuo vya michezo

  1. Uwekezaji katika nishati:

Wilaya imegawanyika katika maeneo ya ukanda wa juu na ukanda wa chini (tambarare).  Katika ukanda wa tambarare kuna upepo mwingi muda wote unaoweza kutumika kwa kuzalisha umeme kwa Teknolojia ya wind mill.  Hii ni fursa nzuri ya uwekezaji katika Wilaya ya Hai.

  1. Uwekezaji katika mashamba ya Ushirika:  Wilaya ya Hai ina jumla ya mashamba 17 yanayomilikiwa na vyama vya ushirika vya mazao.  Mashamba hayo ni makubwa na ni fursa nzuri ya mwekezaji ambapo wawekezaji wanaingia mikataba na vyama vya ushirika ambao ni wamiliki.


FURSA YA UWEKEZAJI SEKTA YA MIFUGO  

1. Ujenzi wa kiwanda cha kusindika maziwa: 

Kiwanda hiki kitawezesha kusinjdika maziwa yanayozalishwa na wakulima wadogowadogo, kitakuwa na uwezo pia waa kuhudumia Wilaya za jirani zikiwemo Siha, Meru, Simanjiro na Moshi Vijijini.

2. Kujenga machinjio ya kisasa:

Uchinjaji katika mazingira bora, utaimarisha afya za walaji kwa kuepusha magonjwa yanayotokana na mazingira machafu kuchina na kutunzia nyama.

Machinjio hii itakuwa na sehemu ya kuchinjia wanyama wakubwa na wadogo, pia kuku.

3. Uzalishaji wa majani yaliyokaushwa na kufungwa:

Uzalishaji unaweza kufanyika katika mashamba makubwa yaliyotaifishwa na kupewa vyamavya ushirika kuyaendesha.   Majanii hayo yatahitajika sana katikaa kuzalisha mziwa kwa wafugai wadogo wa ng’ombe wa maziwa.  Aidha yataweza kuuzwa katikaWilaya za jirani na kuongeza kipato kwa wakulima.  Vile vil itawezesha upatikanaji wa ajira.

4. Kuanzisha vikundi vya kusindika na kutengeneza bidaa za ngozi.

 

FURSA ZA UWEKEZAJI - IDARA YA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA

  1. Econ – tourism – Picnics

Waterfals/ Springs; Kijiji cha Nshara na Chemka.

Forest walking/ Pedestrian travel

Watching birds

Scenic beauty

Historical sites; Rebman tower at Machame, Churches, Mosques

  1. Parks [bustani za mapumziko]
  2. Ufugaji nyuki katika maeneo ya msitu wa hifadhi [ Organic honey production]
  3. Fisheries; Farm fishing, Sport fishing [Maji yaliyopo kwenye mito na mifereji ya umwagiliaji iliyopo].
  4. Eneo la EPZ kwa ajili ya kuzalisha ajjira kwa vijana na jamii kwa ujumla

 

FURSA ZILIZOPO KATIKA KITENGO CHA UTAMADUNI NA VIJANA

 

  1. UWANJA WA MPIRA  [HAI STADIUM]

Halmashauri ina kiwanja kikubwa kinachoweza kupimwa viwanja vya michezo mingi. Kiwanja hiki kipo kwenye eneo lililopimwa na wananchi wamejenga nje ya kiwanja hicho – uwanja huu haujasawazishwa. Fursa hii tunaweza kuitumia kwa kujenga uwanja huo kwa kuzungushia ukuta kwa nje na tukawagawia watu maeneo ya kujenga vibanda vya Biashara ambavyo vinaweza kuingizia Halmashauri mapato. Pia watu wanataka kuingia kufanya mafano; mikutano, micchezo – watatoa kiingilio.

  1. Mji wa Bomang’ombe unaendelea kuwa na vijana wengi wanaohitaji kufanya shughuli za burudani, pia wananchi wanahitaji maeneo ya kupumizika siku za Jumamosi na Jumapili.

Tunalo eneo la kutosha kujenga kituo cha burudani – [Recreational centre] au kujenga kituo cha vijana cha kuonyesha sanaa zao siku za mwisho wa juma [weekends]

Eneo la ‘Green Belt’ lililopo kati ya TANESCO na majengo ya KNCU, tunaweza kutumia eneo hilo bila kuathiri uoto/mazingira ya eneo husika hatimaye tukapata sehemu ya kupumzikia watu baada ya kuzungushia uzio utakaosaidia kupaweka salama wakati wa matumizi.

Eneo hili linaweza kuingizia Halmashauri fedha nyingi kwani kila atakayeingia katika eneo hili atagharamia kwa kiingilio maalum kitakachowekwa na Halmashauri.

FURSA ZILIZOPO KATIKA IDARA YA ELIMU SEKONDARI

  1. Miradi ya upandaji wa miti ya mbao katika maeneo ya shule za Sekondari.
  2. Miradi ya Ufugaji wa samaki katika maeneo wazi ya shule za Sekondari ambazo zipo maeneo yenye maji ya kutosha.
  3. Shughuli za kilimo cha mazao ya chakula na mbogamboga katika maeneo ya shule za Sekondari.
  4. Kuanzisha maduka madogo madogo (vioski) katika maeneo ya Shule.
  5. Saluni za kunyoa nywele pamoja na viwanda vidogo vidogo vya ushonaji katika maeneo ya shule (mf. Ushonaji wa sare za shule).
  6. Kuanzisha shughuli za useremala katika maeneo ya shule (utengenezaji wa madawati).

Kuanzisha Hosteli kwa ajili ya wanafunzi wanaotoka mbali hasa wasichana.

FURSA ZA UWEKEZAJI SEKTA YA AFYA 

Idara ya Afya inatoa huduma za Afya fursa zinazolengwa ni za kutna huduma za tiba (Curative Service), kuzuia magonjwa (Preventive service) na matunzo baada ya kupata madhara (Rehabilitative services).

Hadi sasa wilaya ina vituo vya huduma 60, kati ya hivyo  31 ni vya seerikali na 29 ni vya  watu binafsi na mashirika ya dini.

Mahitaji ya watumishi wa afya ni makubwa, vipo vyuo viwili vya afya (TABIBU NA UUGUZI) vyenye uwezo wwa kudahiri wanafunzi 90.  Hivyo upo uhitaji mkubwa wa vyuo vya afya kada ya maabara na famasia.  Upo uhitaji mkubwa wa kituo cha kufanya uchunguzi wa magonjwa (Diagnostic centre) katika mji wa Bomangg’ombe ambapo kuna vituo Vinci hasa vya binafsi na hakuna huduma hiyo.

Hivyyo fursa za uwekezaji ni katika nyanja zifuatazo:-

  1. Ujenzi/uendeshaji wa vyuo  vya afya kakda ya Maabara na Famasia.
  2. Uwekezaji wa Kituo cha kugundua magonjwa (Diagnostic centre)
  3. Ujernnzi wa kituo cha matunzo ya wagonjwaa wa akili na kifafa (Mental Health Unit).

STRENGTH: (Nguvu, Uwezo, Fursa)

  1. Ujuzi na waledi wa mtumishi
  2. Mtawanyo mzuri wa vituo vya kutolea huduma za Afya
  3. Uwepo wa vituo na vifaa vya kufanyia kazi

WEAKNESS (Mapungufu)

  • Kukatika kwa umeme mara kwa mara katika hospitali ya wilaya kutokana na uunganishaji duni wa mfumo wa umeme.
  • Uingizaji duni wa takwimu katika mfumo wa utoaji wa taarifa za afyaa
  • Ukosekanaji wa vifaa/miundo mbinu kama Maxine ya mionzi, gari la wagonjwa, maabada, stoo ya Dawa na nyumba ya kuhifadhia maiiti katika hospitali ya Wilaya,
  • Ukosefu wa miundo mbinu maalum ya uzoaji taka na utupaji
  • Kutokuwepo kwa usimamizi wa mara kwa mara katika vituo vya kutolea huduma za afya pia ujuzi mdogo wa shughuli za usimamizi kwa baadhi ya wajumbe wa kamati ya usimamizi Wilaya.
  • Kutokujittuma kwa baadhi ya watumishi wa Afya pamoja na mtazamo wa hasi kwa wateja.

CHANGAMOTO:

  • Usambazaji wa Dawa na vifaa tiba usioenda na mahitaji pia ukosefu wa mara kwa mara wa dawa na  vifaa tiba toka bohari kuu ya madawa
  • Bajeti ndogo ya ffedha za matumizi mengineyo
  • Fedha haziji kwa wakati
  • Jamii kutokuelewa kwamba vituo vya kutolea huduma ni mali yao.
  • Kutokuwepo umeme kwa kuaminika
  • Usajili hafifu wa Mfuko wa Afya ya Jamii.
  • Upungufu wa wataalam hasa wa maabara katika vituo vya Afya na Zahanati.

FURSA:

  • Idadi nzuri ya vituo binafsi vya mashirika ya dini.
  • Idadi kubwa ya masirika yanayosaidia masuala  yaa Afya ndani ya Wilaya yetu
  • Mawasiliano mazuri na miundo mbinu mizuri inayofanikisha mmfumo wa ruffaa
  • Uwepo wa kutoa huduma za afya waliopewa mafunzo mbalimbali nddani ya jamii.
  • Jamii kuwa na uelewa na ushirikiano katika mafuala ya afya.

Upatikanajki mzuri wa maji safi na umeme. 

 

 

 

FURSA ZILIZOPO IDARA YA FEDHA

  

(i) MLIMA KILIMANJARO

 

Watalii wengi wanaopanda mlima Kilimanjaro hupitia njia ya Machame.

 

Halmashauri ingetengeneza sheria ndogo ya kukusanya ushuru wa wageni wanaopanda mlima Kilimanjaro kupitia njia ya Machame ingejipatia fedha nyingi za kufanya maendeleo wilayani kwetu.

  

(ii) WAWEKEZAJI:

 

Ndani ya Wilaya ya Hai kuna wawekezaji wa aina nyingi, lakini hakuna sheria ndogo zinazo wabana kuchangia miradi ya Maendeleo.  Sheria ndogo zitungwe kuwabana.

  

(iii) BODI ZA MAJI

 

Bodi zinazosimamia Miradi ya maji zinatakiwa zichangie fedha toka kwenye Ada za maji zitakazo tumika kulinda na kuendeleza vyanzo vya maji na mazingira kwa ujumla.  Sheria ndogo inahitajika.

  

(iv) KUWEKEZA (INVESTMENT) (LGLB):

 

Halmashauri kwa kupitia mfuko wa Serikali za Mitaa na vyombo vingine vya fedha inaweza ikachukua mikopo na kuanzisha Miradi mbalimbali mikubwa ambayo itaipatia Halmashauri fedha ambazo zitawapatia wananchi wa Halmashauri huduma zinazohitajika.

 



 

TAARIFA YA MWAKA

MKOA WA KILIMANJARO

 

 DETAILED DESCRIPTION OF SELECTED PARCHELS FOR THE LAND BANK IN KILIMANJARO REGION

NA

H/W

Eneo lilipo

Ukubwa wa eneo

Limepimwa/ Halijapimwa

Mmiliki

Miundombinu iliyopo

Aina ya uwekezaji

maelezo

Maji
Umeme
Barabara
2
Hai
Weruweru Industrial Area
4.80 acres
Limepimwa
M/S General Pharmaceutical 6000 Arusha.
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
4.60 acres
Limepimwa
M/S Njake Enterprises Ltd.
Box 13 Moshi
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
4.60 acres
Limepimwa
M/S Nkibo Wood Lands Co. Ltd.
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
5.00 acres
Limepimwa
Onesmal Fanuel Mushio
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
5.00 acres
Limepimwa
M/S Lobo Investment Co.Ltd
Box 1636, Moshi.
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
5.00 acres
Limepimwa
M/Elyi’s Co.Ltd. Box 8251, Moshi.
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
5.00 acres
Limepimwa
M/S Kibo Food Processing Ltd. Box 920, Moshi.
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
9.00 acres
Limepimwa
M/S Kilimanjaro Waters Ltd.
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
8.12 acres
Limepimwa
M/S Modson Garments Ltd. Box 290, Dar es salaam.
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
7.00 acres
Limepimwa
M/S S.A. Corporation Ltd. Box 372, Moshi
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
13.00 acres
Limepimwa
M/S Bonite Bottles Ltd. Box 1352, Moshi.
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial Area
2.00 acres
Limepimwa
Kimashuku Commercial Centre, Box 15061, Dar es salaam.
Yapo
Upo
Lami
Kiwanda
Linahitaji fidia au kutwaliwa.


Weruweru Industrial complex.
20 acres
Limepimwa
Mkurugenzi Mtendaji (W) Hai.
Yapo
Upo
Lami




Sanya Station
463 acres
Halijapimwa
EPZA
-
-
-

Upimaji na uthamini kwa ajili ya kulipa fidia kwa wamiliki wa asili bado haujafanywa.
 
  


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai