• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

WASILISHO KWA MKURUGENZI NA WATUMISHI WA HAI 12/10/2020 IDARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI

WASILISHO KWA MKURUGENZI  NA WATUMISHI WA HAI 12/10/2020

IDARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI

Idara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ina jukumu la kusimamia shughuli zote za uzalishaji,  Afya na usimamizi wa sheria za mifugo na uvuvi na pia kutoa tarifa mbali mbali za kisekta kwa wadau mbali mbali. Makao Makuu ya Idara ni katika Jengo la Kliniki ya Mifugo ya Wilaya lililopo karibu na Ofisi ya Idara ya maji

Rasilimali watu

Idara ya Mifugo na Uvuvi ina watumishi waajiriwa 27, kati yao watumishi 6 wanafanya kazi Makao makuu, 19 wapo katika Kata na Vijiji, 2 wanafanya kazi ya ukaguzi wa nyama katika machinjio ya wilaya. Pia kuna watumishi 13 wanaofanya kazi kwa kujitolea, kati yao 3 wapo makao makuu na 10 wanafanya kazi katika vijiji.  Wataalamu 39 wa uhimilishaji wa ng’ombe wa maziwa ambao wanatoa huduma ya uhamilishaji baada ya kuwezeshwa ujuzi huo na Halmashauri kwa kushirikiana na vyama vya ushirika vya maziwa na wadau mbali mbali wa maendeleo katika sekta ya maziwa kama SNV, MATCH MAKER, ADGG na LAND ‘O LAKES.

Idadi ya mifugo katika wilaya ya Hai ni kama inavyoo nyeshwa kwenye Jedwali hapa chini

Ng’ombe wa Maziwa wa kisasa
Ng’ombe wa nyama wa  kisasa
Ng’ombe wa kienyeji.
Mbuzi wa Maziwa
Mbuzi wa Kienyeji
Kondoo
Kuku wa nyama (broilers)
Kuku wa mayai
Kuku wa kienyeji
Bata Maji
Bata Mzinga
Bata Bukini
Kanga
Punda
Nguruwe
Ngamia
Sungura
Sili(Simbilisi)Guinea pigs
Mbwa.
Paka
Farasi
48,316
347
61,431
1,837.
67,001
34,357.
56,378.
124,452.
344,683
6,255.
237.
130.
428
1,562
36,820
120
6,547
421.
7,473.
1414
10

 

 

Uzalishaji wa bidhaa za mifugo 

Ng`ombe wa Asili wanafugwa ukanda wa tambarare kwa njia ya ufugaji huria na wanazalisha wastani wa Kg 180 za nyama kwa ng’ombe 1 na wastani wa maziwa lita 3 kwa siku kwa ng’ombe 1, kwa upande wa mbuzi na kondoo wanazalisha Kg 10 hadi 15 za nyama kwa kila 1 na nguruwe wanazalisha Kg 70 hadi 120 kwa mnyama 1.

Ng’ombe wa kisasa wa maziwa wafugwao Ukanda wa Kati na wa Juu kwa njia ya ufugaji wa ndani (Zero Grazzing System) na huwa wanazalisha  wastani wa lita 11.5 za maziwa kwa ng’ombe kwa siku moja ikiwa ni ongezeko la lita 4.5 ukilinganisha na uzalishaji wa lita 7.0 kwa ng’ombe kwa siku za mwaka 2018

Mtamba wa ng’ombe wa Maziwa aliyeshika nafasi ya pili ya ng’ombe bora wa maziwa kikanda maonyesho ya 88  Arusha mwaka 2019

Ng’ombe wanaokamuliwa kwa wastani ni 12,107 ambapo uzalishaji kwa siku ni lita 139,159.5 na kwa mwaka ni wastani wa lita milioni 50.8

Kuna vyama vya ushirika vya maziwa 16 vilivyosajiliwa pamoja na vikundi  8 vinavyojihusisha na biashara ya kukusanya na kuuza maziwa. Vyama vinne ambavyo ni Nronga, Kalali, Marukeni na Ng’uni vinasindika maziwa na kutoa mazao ya maziwa kama siagi, mtindi, Yoba na jibini.

Idara ya Mifugo kwa kushirikiana na Shirika la SNV tuliratibu na kushauri kuunganisha vyama 16 vya ushirika vya maziwa toka Halmashauri yetu na vyama vinne toka Wilaya ya Siha kuungana  na kuunda Muungano wa vyama vya ushirika vya maziwa Mkoa wa Kilimanjaro vikijulikana kama (Kilimanjaro Dairy Co operative Joint Enterprises) kwa kifupi J.E. Kazi za umoja huu ni kuunganisha nyama vya ushirika wa maziwa katika kutafuta soko la pamoja la maziwa, kuwa na sauti moja katika biashara ya maziwa, kutafuta wawekezaji  mbali mbali wa kuwekeza katika sekta ya maziwa, kutafuta na kusambaza pembejeo bora za mifugo ikiwemo malisho na vyakula vya ziada (Concentrates) .

Muungano wa J.E.  kwa sasa umeingia makubaliano na kiwanda cha vyakula vya mifugo cha Harsho kwa oda maalum ya kuzalisha chakula bora cha ng’ombe wa maziwa na kukisambaza katika vyama vyote kwa bei nafuu.

Katika kuharakisha maendeleo kwenye sekta ya mifugo Idara inafanya kazi na wadau mbali mbali wa maendeleo ambao ni kama ifuatavyo:-

Shirika la Maendeleo la Uholanzi ( SNV). Shirika hili linasaidia katika kutoa  mafunzo ya ufugaji bora kwa wafugaji, mashamba darasa ya malisho bora, usindikaji wa maziwa na kutafuta masoko. Pia wamewezesha kila kituo cha maziwa kuwa na TOT (Wakufunzi)  ambao wamepata elimu ya kuzalisha maziwa yalio bora na huwa wanatoa elimu hiyo kwa wafugaji katika vikundi na shirika za maziwa, pia wamesaidia kufundisha vijana  11 juu ya Uhimilishaji wa ng’ombe wa maziwa AI na kuwawezesha vifaa vya kazi pamoja na usafiri, , kushiriki paredi ya ng`ombe wa mziwa Dodoma, kuwezesha unywaji wa maziwa mashuleni na kuwezesha vijana 10 wanaosafirisha maziwa kutoka sehemu za mbali na vituo vya maziwa.

Shirika la Match Maker Associates (MMA)  Shirika hili limewezesha vikundi 6 vya vijana  kufanya kazi kwenye mnyororo wa thamani wa maziwa kwa kuwapa elimu ya kusindika malisho na kuwapa  mashine 6 za kusindika malisho kila moja ikiwa na thamani ya   Tshs. 13 milioni na pia katika kuboresha biashara ya maziwa shirika limewezesha vikundi vitatu vya vijana kumiliki mashine za  Milk ATM 3  moja ipo hapa Bomang`ombe , na mbili Moshi Mjini kila moja ikiwa na thamani ya  Tshs. 16.5 milioni. Mashine hizi kwa sasa zinauza maziwa bora na salama kwa walaji muda wote.

 

Mashine ya kuchakata malisho ya Kikundi cha Vijana Kijiji cha Saawe

Mashine ya kuuza maziwa (Milk ATM)

Shirika la Capacity Bulding for Organizations (CABO). Shirika hili linatoa Elimu ya Uongozi katika Ushirika na kusaidia uhamasishaji wa uundwaji wa  vikundi vya maziwa vijijini na kuwezesha kinamama na vijana walioko kwenye mnyororo wa thamani wa maziwa kuunganisha wafugaji na wauza pembejeo za mifugo kama vyakula, vifaa vya kukamua na kupima na kuhifadhi maziwa.    

Taasisi ya Utafiti wa mifugo Tanzania (TALIRI) kupitia mradi wa Africa Dairy Genetic  Gain (ADGG) kwa Ushirikiano na Halmashauri yetu tuliweza  kufundisha wataalamu 10 elimu ya uhimilshaji wa ng’ombe wa maziwa na kuwanunulia vifaa vya kufanya kazi hiyo  pamoja na usafiri wa piki piki na mitungi ya kuhifadhi mbegu za ngombe  na pia tuliweza kupima Genetic Potantial za ng`ombe wa maziwa katika Wilaya yetu na kutuwezesha kushiriki maonyesho ya ng’ombe bora wa maziwa kitaifa yaliyofanyika Dadoma ambapo ng’ombe wote 6 kutoka Wilaya ya Hai walikuwa ng’ombe bora wa maziwa kati ya ng’ombe 40 walioshiriki maonyesho hayo.

Pia Taasisi imetoa  Hereni zenye namba za utambuzi wa ngombe bora wa maziwa ili kuwezesha  kuingizwa kwenye mfumo wa utambuzi wa ng’ombe bora kwa baadhi ya wafugaji.

 Miundo mbinu iliyopo

Jengo la ofisi ya Idara ambalo pia ni kliniki ya mifugo ya Wilaya. Pamoja na shughuli za kiofisi tunafanya matibabu ya mifugo na upasuaji wa mizoga ili kutambua magonjwa ya mifugo na kutoa ushauri kwa wafugaji. Miundo mbinu mingine ni pamoja na Vituo vya mifugo 10, majosho  9,  Mabirika ya kunywea maji 9.  Vituo 26 vya uhimilishaji ng’ombe wa maziwa, mabucha 154 visima vya kuchinjia mifugo 122, machinjio 1. Idara kwa kushirikiana na wafugaji wa Kijiji cha Sanya Station  tumehamasisha wafugaji na kufufua josho la Sanya Station na kwa sasa linafanya kazi.

Ng’ombe wakitoka kuoga Josho la Sanya Station.

Pia tumeshapata kibali cha kuanzisha mnada wa mifugo eneo la ekari 12 lililotengwa katika Kijiji cha  Sanya Station. Eneo hilo limeshapimwa na ramani ya Ofisi na choo imeshakamilika.  Mchakato wa fedha za ujenzi wa mnada huu unaendelea.

Magonjwa ya mifugo

Magonjwa makubwa yanayosumbua mifugo katika Halmashauri yetu ni Ndigana Baridi, na Ndigana kali.

Magonjwa ya Kiwele (Homa ya kiwele) , upungufu wa madini.  Kimeta FMD, LSD, Rabies, NCD, Fowl pox, Fowl Typhoid, ASF . Wataalamu wanatoa tiba kwa magonjwa haya kila mara yanapojitokeza na pia kutoa chanjo kwa magonjwa ya mlipuko kwa kufuata ratiba za chanjo za mifugo.

 

Wataalamu wa Mifugo wakichunguza ugonjwa wa Homa ya Nguruwe Kijiji cha Nshara

 

 

Changamoto 

Kwa kuwa maeneo ya kufugia ni madogo kuna changamoto kubwa ya kupata malisho ya kutosha kwa ajili ya kulisha mifugo. Wataalamu wamekuwa wakishauri wafugaji kuotesha malisho bora kama vile Majani ya Rhodes, Elephant grass, Guatemala grass, Desmodium, Lucern, Lukina,  calliandra ambayo ni malisho bora na yanakua haraka na pia yanatoa mavuno mengi katika eneo dogo.

Uchakavu wa  miundombinu ya machinjio na majosho ambapo inahitajika ukarabati mkubwa.

 

Ufugaji bora kwa watumishi

Ili kujikwamua na ugumu wa maisha Idara inashauri watumishi kufuga Kuku wa nyama na mayai kwa kuwa ni ufugaji rahisi na una faida ya kupata lishe na kuongeza kipato na pia hutumia nafasi ndogo. Zaidi madawa tiba na chanjo zipo zinapatikana, ramani za mabanda rahisi zipo na wataalamu tupo.

Ufugaji wa samaki wa kisasa

Huu ni ufugaji mwingine ambao ni rahisi na samaki aina ya kambale wanapatikana na wanakua haraka kwani wanaweza kufikia uzito wa Kg. 1 katika umri wa miezi minne.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai