• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mkuu wa Wilaya ya Hai Kutatua Madai ya Walimu

Imetumwa: July 1st, 2019

Mkuu wa wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ameunda kamati maalumu ya kushughulikia madai ya posho za waalimu waliohamishwa vituo vya kazi kutoka shule za sekondari kwenda shule za msingi.

Akizungumza kwenye kikao na watumishi hao wakiwemo walimu kutoka shule za msingi na sekondari kwenye ukumbi wa KKKT Hai mjini kikiwa na lengo la kusikiliza na kutatua changamoto zao ikiwemo kupandishwa madaraja.

Sabaya amesema kamati hiyo itaongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo pamoja na wajumbe kutoka ofisi ya mkurugenzi huku akiwaongezea wajumbe wawili ambao ni afisa TAKUKURU na afisa wa usalama wa Taifa  itakayokuwa na kazi ya kuhakiki vigezo vilivyotumika kuwalipa posho baadhi ya waalimu huku wengine wakiachwa na kushughulikia madai ya posho hizo.

Aidha amewahakikishia waalimu hao kuwa serikali wilayani Hai ipo pamoja nao hasa katika kushughulikia matatizo na kero mbalimbali wanazokumbana nazo na kuwataka kuendelea kutekeleza majukumu yao bila wasiwasi.

Awali akitoa utangulizi wa kikao hicho; Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo amewataka watumishi waliohudhuria kikao hicho kusema yale yote yanayowatatiza na kuwasababisha wasifanye kazi kwa amani ili yatatuliwe na kuboresha utekelezaji wa kazi zao.

“Nichukue nafasi hii mimi kama mwajiri; kuwaomba watumishi wenzangu kutumia kikao hiki kusema yale yote yanayowakwaza ili tuyatatue kwa pamoja kwa ajili ya kuboresha utendaji wa kazi zetu”. Ameongeza Sintoo.

Akichangia mawazo kwenye kikao hicho; diwani wa kata ya Machame Magharibi Martin Munisi amesema walimu ni kada ya heshima sana kutokana na majukumu yao ya kuandaa vizazi vijavyo vya jamii hivyo kutoa rai kwa mamlaka zinazohusika na maslahi ya walimu kuwatendea haki ili kuwafanya watekeleze majukumu yao kwa ufanisi bila manung’uniko.

Mwaka 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Hai iliwahamisha walimu 277 kutoka shule za sekondari ili kusaidia kupunguza upungufu wa walimu kwenye shule za msingi zoezi ambalo lilikamilika na kuacha mapungufu kadhaa ikiwemo malipo ya posho kwa baadhi ya walimu waliohamishwa.


Mkurugenzi






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai