• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Wanaume Watakiwa Kujitokeza Kuipima Afya Zao

Imetumwa: December 1st, 2022

Afisa tawala wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Mary Mnyawi amewasihi wanaume kujitokeza kupima afya kwa pamoja na wake zao huku akiwataka kuacha kutegemea majibu ya wake zao pale wanapokwenda kupima afya hasa wakati wa ujauzito.

Mnyawi ameyasema hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani ambayo huadhimishwa duniani kote Disemba 01 ya kila mwaka ambapo katika wilaya ya Hai maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya Snow view Bomang’ombe.

“wanaume msitegemee kwamba majibu ya wake zenu wanapokwenda kupima ndiyo majibu ambayo yanatosha kukuonyesha wewe upo salama, na kama yeye je anao? Lakini inawezekana mmoja akapata na mwingine asipate inategemea na kinga ya mtu ilivyo” amesema Afisa tawala Mnyawi

“kwahiyo ninawasihi sana muwe na tabia ya kwenda kupima kwa pamoja ili kuona na kujua afya zetu zikoje ili baada ya hapo pia tuweze kuelimishwa na kujua namna gani ya kuenenda nab ado tunakuwa na muda mrefu tu wa kuishi hapa duniani vinginevyo ni rahisi kudondoka kwa ghafla kwa kuwa hujafanya kile ambacho ungeelekezwa na wataalamu wa afya”

Akizungumzia mapambano dhidi ya Ukimwi, Mnyawi ameeleza kuwa wilaya hiyo imefanikiwa kuwaanzishia dawa za kufubaza makali ya virusi hivyo ARV’s asilimia 94% ya waathirika kati ya 95% ya waathirika waliogundulika kuambukizwa.

Siku ya Ukimwi jumla ya watu 736 walipimwa katika wilaya ya Hai, wanaume wakiwa 242 na wanawake 494 ambapo waliogundulika kuwa na maambukizi ni ya VVU ni 15, wanaume 6 na wanawake 9 hali ambayo inaonyesha kushuka kwa maambukizi kwani waliopima ni wengi ila waliogundulika kuambukizwa ni wachache.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, makamo wa mwenyekiti Halmashauri ya wilaya ya Hai Swalehe Kombo Sway ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya kudhibiti Ukimwi wilayani humo anasema kwamba “tumekaa, tumejaribu kupanua wigo mpana wa kuhakikisha kwamba jamii nzima ya wilaya ya Hai inapata elimu ya kutosha juu ya ugonjwa huo”

Mratibu wa ukimwi hospitali ya Hai Dkt. Macha wakati akitoa taarifa ya hali ya ugonjwa huo ameeleza kuwa kuna mwitikio hasi kwa wanaume kwamba majibu ya wenza wao ndiyo majibu yao, hali ambayo imekuwa ikidhoofisha jitihada za Serikali katika kufikia malengo ya kutokuwa na maambukizi mapya ifikapo mwaka 2030.

Mganga mkuu wa wilaya ya Hai Dkt. Itikija Msuya amewataka wale wote ambao tayari wameambukizwa virusi vya ugonjwa huo kufuata kwa usahihi maelekezo na kanuni za kitabibu ili maisha yaendelee kama kawaida kwani wapo watu wengi ambao wameambukizwa lakini wanafuata maelekezo ya wataalamu wa afya na wanaendelea kuishi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai