• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Watumishi wa Umma Wakumbushwa Kuongeza Uwajibikaji

Imetumwa: July 7th, 2018

Watumishi  wametakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia taratibu za kazi na kuboresha huduma wanazowapatia wananchi ikiwa ni sehemu yao katika kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inaoongozwa na Dr John Pombe Magufuli.

Wito huo umetolewa kwenye ziara ya kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Hai iliyokagua utekelezaji wa shughuli za serikali katika wilaya ya Hai kupitia miradi ya maendeleo inayofanywa na halmashauri.

Akizungumza kwenye ziara hiyo; Katibu wa CCM Wilaya ya Hai Kumotola Kumotola amesema ni jukumu la kila mtumishi wa umma kuongeza ufanisi kwenye eneo lake la kazi ili kuendana na kasi ya serikali katika kuwahudumia wananchi wake.

Kumotola ameipongeza Idara ya Afya kwa kufanikiwa kutekeleza miradi yake kwa kiwango cha kuridhisha ikiwa ni pamoja na kufunguliwa kwa duka la dawa ndani ya hospitali ya wilaya na kukamilika kwa wodi za wanawake.

Kumotola pia amemtaka Mganga Mkuu wa Wilaya kuendelea kudhibiti suala la lugha isiyoridhisha lililokuwa likilalamikiwa na wagonjwa wanaopatiwa huduma katika hospitali hiyo.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Irine Haule ametoa shukrani kwa Rais  Magufuli kwa kutoa vitanda vya kujifungulia kwa wodi za  wajawazito pamoja vitanda vya kulalia wagonjwa wa kawaida huku akiishukuru kamati hiyo kwa kutoa changamoto katika hospitali ambazo zimekuwa zikifanyiwa kazi siku hadi siku na kuisaidia kusonga mbele.

Pamoja na pongezi hizo; kamati hiyo ya siasa imebaini changamoto mbalimbali kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo hali ya uchafu wa mazingira yanayozunguka maabara, utunzaji hafifu wa mali na vifaa pamoja na usimamizi usioridhisha kwa mafundi kwenye mirad ya ujenzi.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Edward Ntakilio amesema kuwa amezipokea changamoto zilizotolewa na kamati hiyo na kuahidi kuzifanyia kazi ili kuboresha ufanisi katika utendaji wa kazi na kuwakumbusha watendaji wa serikali kuwa wanao wajibu wa kuwatumikia wananchi kwa upendo.

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Hai imefanya ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali kwenye wilaya hiyo kwa lengo la kufahamu ni kwa kiasi gani halmashauri inatekeleza miradi kulingana na ilani ya uchaguzi ya chama hicho ambapo ilitembelea ujenzi wa maabara ya shule za sekondari Rundugai na Longoi, ujenzi wa Kituo cha afya Chekimaji,  Kikundi cha uhifadhi mazingira cha Iroko, kikundi cha wakina mama wafugaji ebeneza kilichopo Nronga, jengo la kusindika Vanila, pamoja na hospitali ya wilaya ya Hai.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai