• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

DC Hai Aweka Bayana Muelekeo Kiutendaji

Imetumwa: August 14th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Lengai  Ole Sabaya amewataka watumishi wa Umma wilayani hapo kuongeza juhudi na maarifa katika kuwatumikia wananchi hususani kutatua changamoto zilizopo kwenye jamii.

Sabaya ametoa wito huo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo kwa lengo la kumkaribisha ofisini baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kushika wadhifa huo.

Amesema watumishi wa umma wanatakiwa kukumbuka kuwa wameajiriwa na mwananchi ambaye anatumia nguvu zake kulipa kodi hivyo ni lazima watumishi kuweka mbele maslahi mapana ya wananchi wanaowahudumia badala ya kuangalia maslahi yao binafsi.

Amesema yupo tayari kushirikiana na kila kundi linalohusika kuhakikisha kuwa mwananchi wa Wilaya ya Hai anapata huduma anazostahili ikiwemo elimu, afya, maji, miundombinu na huduma nyingine.

“Nitashirikiana na Katibu wa CCM na Kamati ya Siasa, nitashirikiana na vyama vyote vya siasa vilivyopo, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkurugenzi na watumishi walio chini yake; tukutane tujadiliane namna ya kutatua kero za wananchi badala ya kupoteza nguvu kugombana” ameongeza Sabaya.

Aidha Sabaya ametoa wito kwa wanasiasa hususani madiwani kutumia nafasi walizonazo kusaidia kuwapunguzia wananchi ukali wa maisha kwa kutatua kero mbalimbali walizonazo.

“Kipimo kikubwa kwa wananchi ili uendelee kuwa kiongozi wao sio mavazi, uwezo wa kuongea wala nguvu unazotumia kuwashambulia watumishi wa halmashauri bali wanaangalia namna unavyowasaidia kutatua changamoto zinazowakabili” ameongeza.

Naye Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Hai Kumotola Kumotola amempongeza Mkuu wa Wilaya kwa kuonesha nia ya kushughulika na matatizo ya wananchi kwani Chama Cha Mapinduzi kinachoongoza Serikali ni chama chenye kuwajali wananchi wake.

Amemwomba Mkuu wa Wilaya kutatua kero zinazowasumbua wananchi kwa muda mrefu katika migogoro ya ardhi pamoja na uhaba wa maji hasa kwenye ukanda wa tambarare wa wilaya.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya hafla hiyo Diwani wa Kata ya Bomang’ombe Joel Nkya amesema Mkuu wa Wilaya ametoa hotuba yenye muelekeo inayoamsha matumaini ya wananchi kwa namna anavyojipanga kuwatumikia wananchi kwa kutatua kero zao.

Amesema anayo imani watashirikiana vizuri katika kuwahudumia wananchi wa Wilaya hiyo huku akibainisha kuwa wamepokea wito wa Mkuu wa Wilaya wa kushauriana namna ya kuboresha huduma kwa wananchi.

Kwa upande mwingine Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo amebainisha furaha yake kupata kiongozi wa wilaya na kwamba ofisi yake na watumishi walio chini yake watampa ushirikiano na watamuunga mkono katika kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika kuwahudumia wananchi na kuwaletea maendeleo.

Sintoo amesema amepokea maagizo yaliyotolewa na kiongozi wa wilaya na kwamba yeye na wataalamu walio kwenye ofisi yake wao wajibu wa kutekeleza maagizo hayo kwa manufaa ya wananchi wanaowahudumia.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai