• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

DC Hai: Wazazi Wapelekeni Watoto Kupata Chanjo

Imetumwa: April 27th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Onesmo Buswelu amewataka wazazi wilayani humo kuitikia mwito wa kuwapeleka watoto wao kupatiwa chanjo ili kuwakinga na magonjwa mbalimbali wanapofikisha umri wa kupatiwa chanjo hizo.

Ametoa rai hiyo wakati wa kuzindua utoaji wa chanjo ya sindano ya ugonjwa wa Polio kwa watoto wenye umri wa wiki 14 pamoja na chanjo ya Saratani ya Mlango wa Kizazi inayotolewa kwa wasichana wenye umri wa miaka 9 uliofanyika kwenye hospitali ya Wilaya ya Hai leo 27/04/2018. 

Akizungumza na wananchi waliofika hospitalini hapo na watoto wao kupata chanjo ya ugonjwa wa Polio kwa sindano, Buswelu amesema wapuuze upotoshaji unaofanywa na baadhi ya watu wanaotaka kuwapotosha na kuwasababishia kuwakosesha watoto wao haki ya kuishi bila magojwa kwani chanjo hii inamkinga mtoto na magonjwa ya kupooza.

Aidha Buswelu amezungumzia chanjo ya Saratani ya Mlango wa Kizazi wanayopatiwa wasichana wa umri wa miaka 9 akisema kuwa siyo kitu kipya mkoani Kilimanjaro kwani ilianza kutolewa tangu mwaka 2014 na ilitolewa kwa wasichana wa miaka 9 hadi 14 tofauti na mikoa mingine ambayo chanjo hiyo inaanza mwaka huu.

Biswelu pia amewakumbusha watumishi wanaotoa huduma za afya kutimiza jukumu lao kuu la kuwapatia chanjo walengwa na wasisimamie kwenye kufikisha lengo la takwimu pekee lakini pia kuzitunza kwani zimepatikana kwa fedha nyingi.

“Chanjo hii hatulipii chochote sisi wenye watoto; lakini serikali inagharamia fedha nyingi kwa ajili ya watoto hawa. Kodi zetu zinazokusanywa na serikali ndizo zinazotumika kupata chanjo hii. Serikali ipo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wake”. Amesisitiza Buswelu.

Akitoa utangulizi kuhusu chanjo hizo; Mratibu wa Chanjo Wilaya ya Hai Michael Ndowa amesema kuwa chanjo ni njia madhubuti ya kudhibiti magonjwa kwani kuipata kabla ya maambukizi kunamuepusha mhusika kupata maambukizi ya ugonjwa lakini pia  haina gharama kwa mwananchi kwani inagharamiwa na serikali kwa asilimia mia.

Ndowa amesema kuwa jumla ya vituo 62 vya huduma za afya na shule za msingi 128 katika wilaya vitatumiwa katika kufanikisha kazi ya kutoa huduma za chanjo hizo ambapo kwa wasichana wanaopatiwa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi watafikiwa shuleni na kupatiwa huduma hiyo.

Kwa upande wake kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Hai Dkt. Irene Haule amewakubusha viongozi wa dini na viongozi wa kijamii  kutimiza wajibu wake kwa kuhamasisha na kuhakikisha kila mtoto anayefikisha miezi 14 anapelekwa kupata chanjo hiyo lakini pia wasichana wa miaka 9 waliopo shuleni na wale ambao hawasomi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai