• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

DC Sabaya Aingilia Kati Mwili wa Marehemu Ulioshikiliwa KCMC

Imetumwa: May 8th, 2021


Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya leo Mei 8, 2021 amemuagiza Katibu Tawala wa wilaya hiyo Upendo Wella kusimamia zoezi la kuchukua mwili wa  Bauda Nkya (68) mkazi wa Kijiji cha Nshara kata ya Machame Kaskazini ambaye mwili wake umezuiliwa chumba cha kuhifadhia maiti hospitali ya KCMC kwa kukosa fedha za matibabu.

Sabaya ametoa maagizo hayo alipofika nyumbani kwa marehemu Bauda Nkya kwa lengo la kusikiliza malalamiko ya wananchi wa Kijiji cha Nshara waloonesha kuhuzunishwa na kitendo cha mwili wa mpendwa wao kuzuiliwa.

Waombolezaji hao wamedai kuwa mwili wa mpendwa wao ulizuiliwa katika hospitali ya KCMC baada ya familia yake kushindwa kulipa malipo ya huduma za matibabu waliyokuwa wakidaiwa na hospitali hiyo na kuamua kuchangisha fedha na kufikisha shilingi milioni moja na laki mbili (1,200,000).

 

"Poleni kwa msiba na hongereni kwa kuweza kuchangia kiasi cha shilingi milioni moja na laki mbili; huu ni mfano mzuri wa ushirikiano. Kiasi kilichobaki ofisi yangu itagharamia ikiwa ni pamoja na kufanikisha mwili kuruhusiwa huko uliposhikiliwa.” Amesema Sabaya.

“Mambo mengine ni ya kibinadamu tu, Bibi huyu (marehemu) alikuwa ni mnufaika wa TASAF na hali ya hapa kwake inaonekana, kupata shilingi milioni 3  ni  shida nyingine kwa familia hii, hivyo Mwenyekiti wa Kijiji utashirikiana na DAS (Katibu Tawala Wilaya) kutoka ofisi yangu kufanya taratibu zote na kesho Mei 9.2021 mwili upumzishwe" Ameongeza DC Sabaya.

 

Kwa mujibu wa mtoto wa marehemu Muzaimata Urassa ameeleza kuwa mama yao alikuwa akisumbuliwa na mguu baada ya kujikwaa kwenye kisiki na  kupelekea mguu wake kuoza ambapo alifariki Mei 2 mwaka huu na mwili kuchukua wiki moja bila kuzikwa kutokana na changamoto ya familia kukosa fedha.

Tukio hilo limeleta simanzi zaidi kwa familia na waombolezaji ambao wamesema kuwa mwili wa marehemu ulipaswa kusitiriwa mapema ikiwa pia ni kwa mujibu wa imani yao ya dini ya Kiislamu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali ya KCMC Dkt Gilead Masenga alipopigiwa simu kuzungumzia tukio la kuzuiliwa kwa mwili huo; amesema kuwa hawajawahi kupokea maombi kutoka kwa familia hiyo na kubainisha kuwa kama familia inashindwa kulipia gharama kama hizo wanapaswa kufuata taratibu zilizopo jambo ambalo halikufanyika.

Taratibu zinazofahamika ni kwa ndugu wa marehemu kuwasilisha maombi ya kupatiwa msamaha wa malipo kupitia afisa ustawi wa jamii wa hospitali hiyo ambaye atajiridhisha maombi ya familia na kuruhusu mwili kuchukuliwa.

Mkuu wa Wilaya ametoa maelekezo kwa hospitali kutumia busara kushughulikia masuala ya ndugu wa marehemu kukosa fedha badala ya kuzuia mwili kwani kufanya hivyo kunaongeza machungu kwa wafiwa.


Matangazo

  • TANGAZO LA UKUSANYAJI NA UZOAJI TAKA HAI MJINI September 27, 2023
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA (PSLE) 2023 WILAYA YA HAI November 23, 2023
  • MAJINA YA WALIOITWA USAHILI NAFASI ZA JESHI WILAYA YA HAI September 06, 2023
  • TANGAZO LA UKUSANYAJI NA UZOAJI TAKA HAI MJINI September 27, 2023
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Mhe Kaijage Awataka Watumishi Kufanya Kazi Kwa Bidii

    November 22, 2023
  • Mkalipa Ataka Viongozi Wa Dini Kufundisha Waumini

    November 08, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Sanya Station Washukuru Ulipwaji Wa Fidia

    October 25, 2023
  • Mkurugenzi Dionis Myinga Aishukuru Kambele Kwa Msaada Wa Sementi

    October 23, 2023
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 27 Hai

    Simu: 0272758441

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai