• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

DCC Yaishauri Halmashauri ya Hai Kuimarisha Vyanzo vya Mapato

Imetumwa: February 16th, 2021

Kamati ya ushauri ya Wilaya (DCC) ya Hai mkoani Kilimanjaro imeishauri wilaya hiyo kubuni vyanzo vipya vya mapato pamoja na kuimarisha vyanzo vya mapato vilivyopo ili kujiongezea uwezo wa kuwahudumia wananchi.

Akizungumza kwenye kikao hicho kilichokuwa na ajenda ya kujadili bajeti ya halmashauri; Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Hai Lawrence Kumotola amesema ili halmashauri iweze kuwahudumia vizuri wananchi kwenye sekta za afya hasa matibabu bure kwa wazee, elimu na sekta nyingine ni lazima kuwe na vyanzo vya uhakika vya kukusanya fedha zitakazofanya huduma hizo.

Ameikumbusha Halmashauri kutekeleza agizo la Serikali la kujenga vituo vya afya kupitia fedha za mapato ya ndani ikiwa ni mkakati wa Serikali kuimarisha utoaji huduma za afya karibu na wananchi huku akibainisha kuwa utekelezaji wa agizo hilo uzingatie maeneo yenye uhitaji zaidi.

Kumotola ametumia kikao hicho kuelezea umuhimu wa kituo cha Redio Boma Hai inayomilikiwa na halmashauri hiyo kuwa inaweza kuwa chanzo kikubwa cha mapato iwapo itafanyiwa maboresho yanayohitajika ikiwa ni pamoja na kuiongezea masafa ili isikike kwenye eneo kubwa na watu wengi zaidi.

Kuhusu uanzishwaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Bomang’ombe; Kumotola ameshauri kufanyike juhudi za makusudi za kupata mamlaka kamili ya mji mdogo huo.

Kikao hicho pia kimeipongeza halmashuri ka namna inavyoendelea kutekeleza majukumu yake ya kuhudumia wananchi, maboresho kwenye sekta ya afya baada ya uzinduzi wa kitengo cha kinywa na meno, Kushika nafasi ya nne kitaifa kwenye matokeo ya mtihani ya Darasa la Saba mwaka 2020, Mamlaka ya Mapato (TRA) Wilaya ya Hai kwa kufanya vizuri kwenye makusanyo ya mapato.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo amekiambia kikao hicho kuwa halmashauri yake inapokea ushauri uliotolewa na wajumbe na kwamba wataufanyia kazi ipasavyo kulingana na mazingira ili kuimarisha ufanisi na utoaji huduma kwa wananchi.

Sintoo amesema kuwa halmashauri inasubiri maelekezo ya Serikali kuhusu vyanzo vya mapato vilivyorudishwa kukusanywa na halmashauri ili kuona namna ya kutumia fedha hizo kuboresha huduma za halmashauri ikiwemo ujenzi wa kituo cha afya na huduma nyingine.

Awali akiwasilisha makisio ya bajeti Afisa Mpango wa halmashauri hiyo Herick Marisham amesema makisio ya bajeti ya halmashauri ya Shilingi 34,766,644,328.00 zitakazopatikana kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mapato ya ndani, ruzuku ya mishahara, miradi ya maendeleo na vyanzo vingine pamoja na maombi maalumu ya shilingi 1,345,000,000.00 kwa ajili ya kuhudumia shughuli za halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022.  

Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya kimekaa chini ya kaimu Mwenyekiti Upendo Wella ambaye ni Katibu Tawala Wilaya akimwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo na wamejadili masuala yanayohusu bajeti ya halmashauri hiyo pamoja na bajeti ya TARURA na kushauri namna ya kuimarisha makusanyo pamoja na kuboresha huduma kwa wananchi.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai