• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Elimu Bure Isiwe Kisingizio kwa Wazazi Kukwepa Majukumu Yao

Imetumwa: April 10th, 2019

WAZAZI na walezi wa wanafunzi katika wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro wametakiwa kutotumia kigezo cha serikali kutoa elimu bila malipo kuacha kuwahudumia watoto wao kwa  mahitaji mengine wawapo shuleni.

Akizungumza na wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika shule ya Sekondari Sawe mwisho wa wiki; Afisa Elimu Sekondari wa  Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Julias Kakyama amewataka wazazi na walezi kuendelea kuwahudumia watoto wao kwa mahitaji mbalimbali yaliyo nje ya ada.

Kakyama amewakumbusha wazazi na walezi kuwa bado wanao wajibu wa kuwahudumia watoto wao wakiwa shuleni kwa mahitaji ya chakula na sio kuwashindisha njaa kwa kisingizio cha kwamba serikali inatoa elimu bure.

Amesema kuwa serikali imeamua kutoa elimu bure lakini haijakataza wazazi au walezi kuwahudumia watoto wao mahitaji mengine kama vile sare za shule, chakula, ulinzi wa mtoto pamoja na kufuatilia maendeleo ya watoto wawapo shuleni.

Amefafanua kuwa wazazi na walezi wanapaswa kuhakikisha kuwa watoto wanapata chakula wawapo shule ili kuwawezesha kumudu vipindi vyote vya masomo darasani na kwamba kuwapatia watoto chakula kunasaidia kuzingatia masomo na kuongeza kiwango cha ufaulu.

“Katika mpango wa elimu bila malipo wazazi na walezi wajitahidi kutimiza wajibu wao wa kuwahudumia watoto huduma zile muhimu ikiwemo kuwanunulia madaftari, sare za shule na kuhakikisha kuwa wanapata chakula shuleni ”amesema Kakyama.

Amesema serikali ya awamu ya tano imefuta ada pamoja na michango mbalimbali iliyokuwa kero kwa wazazi na walezi ili kila mtoto wa kitanzania apate elimu kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne bure, wawazi wanapaswa kuwahudumia watoto mahitaji mengine.

“Kwa sasa wazazi hamlipi tena ada wala michango; wajibu wenu ni kununua sare za shule na kununua mahitaji mengine kama kalamu, daftari na mabegi, Serikali inaendelea kuhamasisha mtimize wajibu kwa kuwanunulia watoto wenu sare hizo” ameongeza.

“Tunaomba mtimize wajibu wenu kuchangia chakula shuleni kwa sababu tunapotoa chakula shuleni tunapunguza utoro, tunaongeza umakini na ufuatiliaji kwa wanafunzi pale wanapofundishwa, wanafunzi wengi wao wanatoroka pale wanapohisi njaa na wakiondoka baadhi yao hawarudi” amesema afisa elimu huyo.

Hata hivyo Kakyama amehimiza wazazi kusimamia ipasavyo maadili ya watoto wao ili waweze kufanikiwa na kufikia malengo waliyojiwekea kitaaluma kwa kushirikiana na walimu katika kuhakikisha watoto wanakuwa na nidhamu ya kuridhirisha katika jamii inayowazunguka.

Pia amewataka walimu na wazazi kuhakikisha wanawasisitiza wanafunzi kutii sheria za shule ikiwemo uvaaji wa sare sahihi ya shule, kuheshimiana na kutumia lugha nzuri wanapowasiliana.

“Wazazi tuna jukumu kubwa la kusimamia suala la maadili ya watoto wetu, suala ambalo huwezi kulitenganisha na mafanikio bora kitaaluma kwani mtoto wenye nidhamu na maadili mema daima hufanya vizuri darasani na yule asiye na nidhamu huporomoka katika taaluma. Nasisitiza nidhamu na taaluma huenda pamoja, haiwezekani kuvitenganisha hata mara moja.” Amesisitizi Kakyama.

Akichangia kwenye mkutano huo mmoja wa wazazi waliohudhuria ameshukuru kwa kuelimishwa kuhusu nafasi ya mzazi katika kufanikisha elimu ya watoto wao akibainisha kuwa wazazi bado wanahitaji kuelimishwa na kukumbushwa mara kwa mara kuhusu mgawanyo wa majukumu hasa yanayowahusu wazazi katika elimu bila malipo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Ujenzi Wa Bweni La Shule Ya Machame Kukamilika Kabla Ya June 19

    May 29, 2025
  • Vijana Wasauriwa Kutumia Fursa

    May 27, 2025
  • Wafanyabiashara Wa St Stend Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Wafanyabiashara Wa Send Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai