• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Jamii Yatakiwa Kutembelea Vivutio Vya Utalii Vya Ndani

Imetumwa: October 21st, 2022

Utalii wa ndani umekua ukihimizwa na viongozi mbalimbali ikiwemo wa Halmashauri ya wilaya ya Hai ikiwa njia nzuri ya kuongezea Taifa pato pamoja na kuthamini rasilimali za taifa.

Hayo yamebainika baada ya timu ya wataalam halmashauri ya wilaya ya Hai kutembelea eneo linaloitwa Sieni lilipo Masama katika ziara iliyolenga kutembelea vivutio mbali mbali vya utalii kwa lengo la kuangalia namna ya kuviboresha na hatimaye kuanza kutumika.

Akizungumza katika ziara hiyo Afisa utalii wilaya ya Hai  Amani Temu amesema  vivutio hivyo vya utalii ni  muhimu kwa wilaya ya Hai endapo vitaboreshwa kutokana na historia ya eneo hilo kuwa ni ya kipekee kwani kuna eneo ambalo linaitwa daraja la mungu ambalo ni daraja lililojijenga lenyewe kwa mawe pekee.

“pamoja na huu uzuri unaonekana hili daraja likiwekewa vizuizi ili mtu ajishike asione kizunguzungu litatuingizia sana kipato kwasababu watalii watatamani kuja hapa kuona hilo daraja la mungu lipoje na kwanini liitwe hivyo kuna historia gani hapa  hiyo ni hatua tosha ya kuongeza pato la nchi kwa watalii wa ndani na wa nje wakija hapa kuona daraja hili, kwakweli tuthamini vya kwetu”.

Miongoni mwa wa watu waliokuwa kwenye ziara hiyo ni mchungaji Walter Kimaro aliyeishi katika  eneo hilo kwa muda mrefu na kuelezea kuwa eneo hilo ni sehemu ambayo watu walikuwa wanaenda kufanya ibada na kuomba baadhi ya vitu huku wakienda wakati mwingine wanavikuta.

Ameongeza kuwa eneo hilo lilikuwa na mapango ambayo watu walikua wanajificha  wakati wa vita vya wenye kwa wenyewe(wamachame na wakibosho).

Pia eneo hilo lilikuwa likitumika  kuangalia utabiri wa matukio ya mwaka kama vile njaa, ugonjwa, ukame pamoja na mvua lakini kwa zama za sasahivi hicho kitu hakipo tena.

“nilifahamu eneo hili mwaka wa 61 nikiwa mdogo sana kipindi hicho ukitaka kuongea na mababu lazima uingie huko kwenye mapango , walikuwa wanaenda na vitu vya kuchinjachinja na pombe saa nyingine , na sio kila mtu alikua anapaswa kuingia huko ilikua ni watu maalumu  na mpaka ukristo ulipoingia waliacha mila hizo zilionekana hazina maana japo kweli ulikua ukiomba unapata kabisa”.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Hai David Lekei amesema anatambua eneo hilo kama eneo muhimu sana na maeneo kama hayo ni lulu kwa taifa na ni maeneo ya kipekee ya kuweza kutuingizia kipato.

“ tunashukuru sana kwa mapokezi tuliyopata nadhani hili eneo linapaswa liandikiwe historia ili watalii wakianza kuja wapate historia kamili hili eneo ni la kipekee kwakweli siajawahi kuona eneo kama hili nashukuru sana uongozi wa kijiji pamoja na uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Hai kwa kuweza kushirikiana kufahamu sehemu kama hii hivyo tuhimizane tuanze wenyewe kuwa watalii na tuyatunze haya maeneo kwa vizazi vijavyo na kwa Taifa pia kwenye kuongezea pato nchi hili eneo liandikiwe historia kwakweli naomba sana”.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai