• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Kamati ya Siasa Yavutiwa Utekelezaji Miradi ya Maendeleo Wilayani Hai

Imetumwa: February 4th, 2021


Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kilimanjaro imefurahishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo unavyofanyika kwa ufanisi katika Halmashauri ya Wilaya ya Hai

Akizungumza baada ya ziara ya kamati hiyo kutembelea miradi inayotekelezwa kwenye halmashauri hiyo; Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro na Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa huo Zuhura Chikira amesema amefurahi kuona matumizi mazuri ya fedha za Serikali katika kutekeleza miradi.

“Nimeona kazi nzuri inayofanywa na kila mmoja kwa nafasi yake; Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi na wataalamu wake bila kusahau chama”

“Binafsi nimeridhika kwa ufanisi niliouona hasa matumizi sahihi ya fedha za Serikali kutekeleza miradi inayoonekana yenye ubora na kuonesha thamani halisi ya fedha zilizotumika. Nitafikisha salamu zenu kwa chama chetu ngazi ya Mkoa hadi ngazi ya Taifa” amesema Chikira.

Naye Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa anayetokea Wilaya ya Hai Yassin Lema pamoja na kupongeza mafanikio ya utekelezaji wa miradi amewakumbusha viongozi wa chama na serikali kuendelea kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli za maendeleo ili kuongeza kasi ya maendeleo.

“Viongozi wa chama na halmashauri waendelee kuelimisha wananchi umuhimu wa kuchangia shughuli za maendeleo hasa ikizingatiwa tulikotoka kuna wenzetu waliwaambia wananchi kuwa serikali inafanya kila kitu hivyo kupunguza ushiriki wa wananchi” Amesisitiza Lema.

Naye Mjumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Hai ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo na Diwani wa Kata ya Muungano Edwin Rutaraka ameonesha kuridhishwa na hali ya utekelezaji wa miradi hasa kwenye matumizi mazuri ya fedha za Serikali.

“Tumepokea maelekezo yaliyotolewa, kwa sehemu yetu kama chama tutaisimamia Serikali kuona wanatekeleza kama ilivyoelekezwa kwa ufanisi” Amesema Rutaraka.

Akizungumza kwa niaba ya wataalamu wa serikali; Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo ameishukuru kamati ya siasa mkoa kwa kutembelea miradi katika halmashauri yake na kwamba maagizo yaliyotolewa yatafanyiwa kazi kwa ufanisi ili kuboresha huduma kwa wananchi.

Aidha Sintoo amebainisha kuwa anafarijika kufanya kazi na Chama cha Mapinduzi kutokana na umakini uliopo kupitia mfumo wa chama hicho na kuahidi kuendelea kushirikiana na viongozi wa chama katika kuhudumia wananchi.

“Tunaomba wenzetu wa chama na viongozi waliopo kwenye jamii kuhamasisha wananchi kuanzisha miradi. Sisi kama halmashauri tutaendelea kufanya ukamilishaji kwa miradi inayoanzishwa na jamii; wakijenga boma sisi tutaleta vifaa vya kupaua” Amesisitiza Sintoo.

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Kilimanjaro imekagua mradi wa kukarabati shule kongwe za Sekondari ya Lyamungo Sh. 799,443,156, Sekondari ya Wasichana Machame wa Sh. 847,658,579.

Pia kamati hiyo imekagua miradi ya kwenye shule za msingi ikiwemo ujenzi wa chumba kimoja cha darasa Shule ya Msingi Narumu Tella kinachotekelezwa kwa nguvu ya wananchi kwa Sh. 1,187,000. Ujenzi wa vyumba 4 vya madarasa na matundu 5 ya choo kwenye shule ya Msingi Kibaoni unaogharimu Sh. 85,500,000 pamoja na ujenzi wenye thamani ya Sh. 240,413,000 wa vyumba 7 vya madarasa na matundu 8 ya vyoo kwenye shule ya Msingi Kibohehe ambapo Ubalozi wa Japan umechangia Sh. 206,000,000 na nyingine kutoka halmashauri na wadau mbalimbali.

Halmashauri ya Wilaya ya Hai imejizatiti kufanya ukarabati wa mara kwa mara wa shule zake za msingi ili kuziweka kwenye mazingira bora ya kufundisha na kujifunzia na hatimaye kuongeza ufaulu wa wanafunzi.  



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai