• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Kicheko Kwa Wananchi wa lambo estate, ni baada ya kaya 78 kupewa ekari 156

Imetumwa: October 25th, 2018

“Tunaishukuru sana serikali kwa hatua hii, ni kitu ambacho hatukutegemea kwani tangu mwaka 1996 mimi mwenyewe nafuatilia suala hili na hatukuwahi kupata suluhu, namshukuru sana Rais John Pombe Magufuli pamoja na serikali yote”

Hii ni kauli ya Saidi Omari miongoni mwa wananchi waliohudhuria kikao  kilichofanyika leo kati ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi na wananchi wa kijiji cha Nshara pamoja  na bodi ya mradi wa umoja wa vyama vitatu vya ushirika vya Foo, Nronga na Wari katika shamba la Lambo Estate.

Katika kikao hicho Waziri Lukuvi ameagiza kaya 78 za wananchi waliokuwa wafanyakazi wa mashamba ya mkonge (Lambo Estate)  wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro kupewa ekari 156 ikiwa ni  utatuzi wa mgogoro kati ya wananchi hao na mradi wa umoja wa vyama hivyo.

Agizo hilo limekuja baada ya mgogoro wa shamba la Lambo Estate na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Nshara ulionza tangu miaka ya tisini baada ya wanachi hao kutuma maombi serikalini wakiomba kupewa eneo la makazi ikifuatiwa na tukio la ajira yao kukoma   ambapo mwaka 2001 wafanyakazi hao walifungua kesi kwa kutoridhika na stahiki walizolipwa na mradi huo.

Mwaka 2003 Mahakama iliamuru wafanyakazi hao  waendelee kuishi kwenye nyumba za ushirika na wapewe hekari 50 kwa ajili ya kuwawezesha kufanya shughuli za kilimo pasipo kujenga makazi ya kudumu.

Akizungumza na wananchi pamoja menejimenti ya  bodi ya vyama hivyo Waziri Lukuvi amesema serikali ya Awamu ya Tano haiwezi kuona wanyonge wakiendelea kuteseka kwa sababu  ya watu  wachache na kwa sababu hiyo imeagiza wananchi hao wasifukuzwe  katika eneo hilo.

“Hamuwezi kujikusanya huko wajanja wachache na kutaifisha ardhi za vijiji alafu mnawakodisha wananchi ardhi na kutumia fedha hizo, huu ni ukoloni kabisa safari hii tutanyoosha maneno yote haya yaliyopinda kwani serikali hii ya awamu ya tano haitacha  mambo haya yapite hivi” amesisitiza Lukuvi.

Kufuatia hatua hiyo  amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya kusimamia zoezi la upimaji wa ardhi  hiyo ili kuziwezesha kaya hizo kupata hekari 2  kwa ajili ya makazi na  shughuli za kilimo na uzalishaji wa chakula kwa masharti ya kutouza maeneo watakayopewa.

Katika hatua nyingine Waziri Lukuvi ameuagiza uongozi wa NDC kulipa kabla ya mwezi Disemba kodi ya ardhi ya eneo wanaolimiki na kufanyia kazi tangu walipokabidhiwa eneo hilo ili kuwawezesha kupewa hati miliki ya eneo hilo na endapo hawataweza kufanya hivyo taratibu za kulirudisha eneo hilo kwa serikali.

Akizungumza katika eneo hilo la machine tools ameagiza wananchi wote waliomilikishwa maeneo katika eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ya ekari 1000 na wameshindwa kuliendeleza wapewe notisi ya siku tisini ili taratibu za kuchukua eneo hilo  na kwa wale waliopimiwa na hawana hati ya umiliki orodha yake ifikishwe kwake na wapewe taarifa ya kutokuwa na umiliki wa eneo hilo.

“Asiye na hati niorodhesheni tu nitatoa idhini ili tutangaze watanzania wengine na wawekezaji wageni wenye uwezo wa  kuwekeza waje wawekeze, eneo hili limekaa muda mrefu pasipo kuendelezwa na lipo mjini”

Naye Mkuu wa Wilaya ya Hai  Lengai Ole Sabaya amemweleza Waziri kuwa amepokea maagizo yote yaliyotolewa kwenye ziara hiyo na kuweka bayana kuwa atayatekeleza kwa nguvu zote ili haki ya kila mhusika ipatikane lakini pia kuiwezesha serikali kukusanya mapato stahiki kutokana na kodi zitakazolipwa kwenye maeneo hayo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai