• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mafanikio ya Awamu wa Tano katika Wilaya ya Hai

Imetumwa: February 3rd, 2019

Serikali imetoa kiasi cha shilingi  5,558,604,325.95 kwa ajili ya kugharamia elimu bila malipo kwa Wilaya ya Hai kuanzia Desemba 2015  ambapo kati ya fedha hizo shilingi  1,633,980,574.16 zimetumika  kugharamia elimu bila malipo kwa shule za msingi na 3,924,623,751.79  kwa ajili ya kugharamia elimu bila malipo kwa kidato cha kwanza hadi cha nne.

Hali hiyo  imesababisha ongezeko la uandikishaji wanafunzi ngazi ya awali kutoka 3,843 mwaka 2015 hadi kufikia 4,127 mwaka 2018 na msingi kutoka 4,201 mwaka 2015 hadi kufikia 4,758 mwaka 2018.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwa miaka mitatu katika wilaya ya Hai, Mkuu wa Wilaya hiyo Lengai Ole Sabaya amesema sera ya elimu bila malipo kwa watoto wenye umri kwenda shule imefanya watoto wengi kutoka kwenye familia duni kupata fursa hiyo muhimu kwa ajili ya maendelo ya taifa.

Alisema serikali imeendelea kuboresha mazingira ya ufundishaji na ufuatiliaji wa shule ambapo kwa mwaka 2018 Wilaya ilikabidhiwa  pikipiki 17 kwa ajili wa waratibu elimu kata ikiwa ni sambamba na uboreshaji wa miundo mbinu ya elimu ikiwemo ujenzi wa vyumba 35madarasa  ya elimu msingi, matundu 120 ya vyoo.

Aliongeza kuwa Wilaya imepokea  walimu 22 wa masomo ya sayansi na kuongeza idadi ya walimu kutoka 118 hadi walimu 140 katika juhudi za kuimarisha masomo ya sayansi shuleni.

“Kutokana na juhudi za serikali kuboresha sekta ya elimu pamoja na usimamizi na ufuatiliaji unaofanywa na viongozi wa ngazi zote, Wilaya ya Hai ilishika nafasi ya pili kimkoa na nafasi ya nane kitaifa katika matokeo ya darasa la saba mwaka jana” Alisisitiza Sabaya.

Mbali na elimu; Sabaya alisema pia serikali imeendela kutoa fedha kupitia mfuko wa maendeleo ya Jamii (TASAF) katika mpango wa kunusuru kaya masikini ambapo hadi Desemba 2018 jumla ya shilingi 3,049,467,299.98 zimetolewa kwa kaya  3,890 walizotumia kuanzisha miradi midogomidogo inayowapatia kipato ikiwemo kufuga kuku, kilimo cha bustani za mbogamboga  na biashara mbalimbali.

Akizungumzia sekta ya Afya; Dc Sabaya alisema kiasi cha shilingi 1,496,355,495.00 zimetumika kununua dawa  na kufanya kiwango cha upatikanaji wa dawa kufikia asilimia 90.57 ukilinganisha na asilimia 73.59 ya  mwaka 2014.

“Tunaendelea kuboresha sekta hii muhimu na tumejenga duka la dawa linalotoa huduma kwa gharama nafuu saa 24 kwa wananchi wa kutoka maeneo mbalimbali nadni na nje ya wilaya” alisema.

“Tumekamilisha wodi ya wanawake katika hospitali ya wilaya, kukamilika kwa miundo mbinu hii muhimu kumewapunguzia wananchi adha ya kutembea umbali mrefu kwa ajili ya kutafuta huduma na kupunguza  idadi ya wagonjwa waliokuwa wanalazimika kwenda Hospitali ya Mkoa Mawenzi’alisisitiza Sabaya.

Katika kuboresha sekta ya umwagiliaji; serikali kwa kipindi hicho imetoa shilingi 844,000,000 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa mifereji 3 ya umwagiliaji ili kuongeza eneo la umwagiliaji kwa lengo la kuimarisha  uzalishaji.

Aidha  wilaya ya Hai imeanzisha  kilimo cha mazao mawili ya biashara ambayo ni Korosho  na vanilla kwa lengo la kuinua uchumi wa mkulima.

Akizungumia huduma ya maji Sabaya alisema serikali imetoa kiasi cha  shilingi 4,062,951,699.35  kuimarisha usambazaji wa maji ambazo zimetumika kufanya ujenzi na upanuzi wa mradi wa maji wa Losaa-Kia, kujenga vituo 58 vya kutolea huduma kwenye vijiji 10 vya Mkalama, Mijongweni, Ngosero, Mbatakero, Mungushi, Kimashuku, Sanya Station, Tindigani, Mtakuja na Chemka.

Naye mgeni wa heshima Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa,  Ndugu Kheri James  alipongeza  ushirikiano ulipo kati ya viongozi wa Wilaya ya Hai na kutaka hali hiyo iendelezwe.

Kheri alisema kuwa juhudi zilizoonyeshwa na waatalamu  kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya na Kamati ya ulinzi na usalama imeifanya Wilaya kuwa ya kwanza Kimkoa na ya kumi kitaifa katika ukusanyaji wa mapato na kwamba hali hiyo itaboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai