• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mbio za Mwenge wa Uhuru Zachangia Ukarabati wa Shule

Imetumwa: September 29th, 2018

Mwenge wa Uhuru umeendelea kufanikisha jukumu la kuangaza Tanzania ikiwa ni pamoja na kuamsha kiu ya maendeleo kwa wananchi wa maeneo unapopita.

Katika Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Mwenge wa Uhuru umefanikisha hilo kwa kuchangia ukarabati wa majengo ya shule ya Msingi Kibohehe ambayo iliezuliwa paa.

Akielezea tukio hilo kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2018, Mkuu wa wilaya ya Hai Nengai Ole Sabaya amesema wamekusanya michango kutoka kwa wadau, watumishi wa umma na wananchi kugharamia shughuli za mwenge na kupata zaidi shilingi milioni 34 na kutumia milioni 30 na laki 9.

Amesema uongozi wa Wilaya umeamua kutumia fedha zilizobaki kununua mifuko 138 ya saruji yenye thamani ya shilingi milioni mbili huku kiasi cha shilingi milioni mbili kikikabidhiwa kwa ajili ya kufanikisha lengo la kuirudisha shule hiyo kwenye hali bora ili wanafunzi waweze kusoma bila bugudha.

Akikabidhi mchango huo wa saruji na fedha taslimu Kiongozi wa Mbio za Mwenge Charles Kabeho ameipongeza wilaya ya Hai na watu wake kwa kutekeleza kwa vitendo dhana ya kuwekeza kwenye elimu kama ilivyo kauli mbiu ya mwaka huu inayohamasisha jamii kuwekeza kwenye elimu kwa maendeleo ya Taifa.

“Nachukua nafasi hii kuwapongeza viongozi wa Wilaya ya Hai kwa kufanya maamuzi sahihi ya kimaendeleo lakini pia wananchi kwa kushiriki kuchangia shughuli za maendeleo” Amesema Kabeho.

“Niwaombe ndugu wananchi muendelee kuchangia maendeleo  kwa michango ya fedha taslimu, vifaa au nguvukazi ili kwa pamoja tushirikiane kuboresha huduma” ameongeza Kabeho.

Aidha Kabeho ameipongeza Wilaya ya Hai kwa kushiriki kikamilifu kwenye Mbio za Mwenge mwaka 2018.

“Wakati wa kukimbiza Mwenge wa Uhuru Wilayani Hai tumefarijika sana kuona namna wananchi walivyojitokeza kuulaki kwenye maeneo ya miradi na maeneo yote Mwenge wa Uhuru ulipopita”

Mwenge wa Uhuru mwaka 2018 umekimbizwa kwenye jumla ya kilometa 98 katika Wilaya ya Hai na kutembelea miradi  ya maendeleo ambayo miradi miwili imezinduliwa na mmoja umewekewa jiwe la msingi yenye thamani ya shilingi milioni 461,649,943.

Miradi hiyo iligusa sekta ya kilimo kwa kuzindua shughuli za kuzindika zao la vanilla, uzinduzi wa duka la dawa katika hospitali ya Wilaya ya Hai pamoja na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa ukuta wa uzio wa shule ya sekondari ya wasichana ya Machame.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA UDEREVA, MWANDISHI MWENDESHA OFISI, MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU NA MHUDUMU WA JIKONI June 02, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Ujenzi Wa Bweni La Shule Ya Machame Kukamilika Kabla Ya June 19

    May 29, 2025
  • Vijana Wasauriwa Kutumia Fursa

    May 27, 2025
  • Wafanyabiashara Wa St Stend Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Wafanyabiashara Wa Send Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai