• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Migogoro ya Wakulima Wafugaji Kupatiwa Ufumbuzi

Imetumwa: October 30th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ameagiza wenyeviti wa vitongoji, vijiji na watendaji kijiji na kata kutopokea fedha zozote zinazotokana na migogoro  kati ya wakulima na wafugaji katika maeneo yao badala yake watoe taarifa ya  migogoro hiyo kwa Mkurugenzi Mtendaji na ofisi ya  Mkuu wa Wilaya.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Sanya Station kata ya Kia Wilayani Hai, Sabaya amesema serikali haiwezi kuvumilia kuona migogoro hiyo ikiendelea na kuwaasa watendaji na wenyeviti kuepuka kuwa sehemu ya mgogoro kutasaidia kwa kiasi kikubwa kumaliza migogoro hiyo.

“Kwa namna yoyote ile serikali haitavumilia unyanyasaji wowote utakaofanywa kwa wafugaji  wala haitavumilia kuona wafugaji wanaonea wakulima, hivyo  ni marufuku kwa wafugaji kuingiza mifugo  kwenye mashamba ya wakulima na kila mkulima abaki katika eneo lake ili kuepuka migogoro.“ Alisisitiza Sabaya.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi  Prof. Elisante Ole Gabriel ameitaka jamii ya wafugaji kufuga kibiashara kwa kuwa na mifugo michache yenye afya nzuri na kutii sheria za nchi  ili kuzua migogoro baina yao na wakulima

Amesema  serikali ya awamu ya tano inawathamini na kuwapenda wafugaji  kwa kuwa wana haki sawa na wakulima na wafanyakazi hivyo nao wanao wajibu wa kutii mamlaka na sheria zilizopo.

Amesema wizara yake inatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambapo ibara ya 25 kifungu a hadi q inawazungumzia wafugaji na kuwaondoa hofu iliyopo miongoni mwao ya kwamba serikali haiwathamini.

“Mhe. Waziri Mpina amenituma niwaambie na niwahakikishie wananchi wa Hai hasa wafugaji   kuwa Rais John Magufuli ni kipenzi cha wafugaji, hivyo amewataka mmtunzie heshima hiyo na mjue kuwa serikali inatambua haki ya wafugaji na mtembee kifua mbele” amesema Prof. Gabriel.

Amesema kuwa mifugo haiwezi kuendelezwa bila ya kuwaendeleza wafugaji kwa kua vyote vinategemeana na kwamba wizara inaendelea kuboresha na kufanyia kazi changamoto za wafugaji kwa kuwa mifugo inachangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa uchumi akitolea mfano wa ng’ombe na mazao yake ambayo imeajiri kundi kubwa la wananchi.

Naye Katibu wa wafugaji nchini  Magembe Mkaoye  ameiomba serikali kuweka mpango wa matumizi bora ili kutenga eneo la kulishia mifugo na eneo la wakulima ili kupunguza migogoro kati ya wakulima na wafugaji.

Ameongeza kuwa wafugaji wanategemea mifugo katika kukidhi mahitaji yao ya kifamilia pamoja na uchumi wao hivyo ameasa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya wafugaji kuheshimiwa ili kuepuka changamoto ambazo zinaarudisha nyuma maendeleo.

Kwa upande wao wananchi waliopata nafasi ya kuzungumza kwa niaba ya wenzao  wameiomba  serikali kuwatengea maeneo rasmi ya malisho na kuwajengea majosho ya mifugo na kuwapa elimu ya kuhudumia mifugo na kutambua magonjwa yanayowasumbua, maombi ambayo katibu Mkuu alihidi yatafanyiwa kazi mapema.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Elisante Ole Gabriel amefanya ziara ya kikazi ya siku moja katika Wilaya ya Hai akiwa na lengo kuu la kufahamu changamoto zinazowakabili wafugaji ikiwa ni hatua ya kuimarisha shughuli za ufugaji nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA UDEREVA, MWANDISHI MWENDESHA OFISI, MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU NA MHUDUMU WA JIKONI June 02, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Ujenzi Wa Bweni La Shule Ya Machame Kukamilika Kabla Ya June 19

    May 29, 2025
  • Vijana Wasauriwa Kutumia Fursa

    May 27, 2025
  • Wafanyabiashara Wa St Stend Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Wafanyabiashara Wa Send Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai