• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mikopo ya Halmashauri Kuwainua Wananchi Kiuchumi

Imetumwa: December 13th, 2018

“Serikali kuwahimiza mjiunge kwenye vikundi ili kuweza kupatiwa mikopo ni namna ya kuwaweka pamoja watu wenye ujuzi na uzoefu tofauti utakaosaidia kuwainua kiuchumi kwa kutumia maarifa tofauti yaliyopo kwenye kikundi”

Hayo ni maneno ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo wakati akifungua  mafunzo kwa vikundi kuhusu namna ya kutumia kwa tija mikopo inayotolewa na serikali.

Sintoo amesema kuwa mikopo hiyo inayotolewa na serikali kupitia makusanyo ya halmashauri ipo na inawahusu wananchi wote ambao wapo tayari kujiunga kwenye vikundi vya uzalishaji mali pamoja na kukidhi masharti na taratibu za kuweza kupatiwa mkopo.

“Serikali inaamini kuwa watu wote wao uwezo wa kufanya kazi za kujiingizia kipato lakini wapo watu wanoshindwa kutimiza hilo kwa kukosa mtaji; mikopo hii inalo lengo kuu la kuinua hali ya kiuchumi ya kila mwananchi kwa kuwapa fursa ya kujitengenezea kipato halali”. Amesisitiza Sintoo.

Awali akizungungumza wakati wa kumkaribisha Mkurugenzi Mtendaji; Afisa Maendeleo ya Jamii Lucas Msele amesema kuwa mikopo hiyo hutolewa kwa vikundi ambavyo tayari vimeshatembelewa na kufanyiwa tathmini na kuona kuwa wanastahili  kupewa mikopo, wanaelekezwa namna  ya kufanya marejesho, elimu ya ujasiriamali pamoja na elimu ya kuweka na kukopa.

Msele amesema kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Raisi Dr. John  Magufuli imeondoa riba kwa vikundi vyote vinapochukua mkopo kutoka Halmashauri lengo likiwa ni kuwaondolea umasikini watanzania hasa wanawake, vijana na walemavu.

Pia Msele amewapongeza watumishi wa idara ya maendeleo ya jamii, watendaji kata na viongozi wa serikali za mitaa kwa kushirikiana kwa pamoja kusimamia vikundi na kuhakikisha vile vinavyokidhi vigezo ndivyo vinavyopatiwa mkopo ili viweze kuzalisha na kurejesha mikopo hiyo.

Kwa upande wao wanavikundi waliopata mikopo kutoka halmashauri ya wilaya ya Hai wameishukuru serikali kwa kuwapatia mkopo usiokuwa na riba na kusema kuwa wamefurahishwa na hatua hiyo na kwamba shughuli za vikundi hivyo zitafanyika kwa ufanisi baada ya mkopo huo usiokuwa na riba.

Katibu wa kikundi cha AGROP kutoka kijiji cha KwaSadala wilayani hapa Clara Njigilile amesema kikundi chake kinashukuru kupatiwa mkopo huo usio na riba na kuahidi kurejesha mkopo huo mapema ili kuwapa nafasi wananchi wengine waweze kukopa.

Naye mwakilishi wa kikundi cha walemavu wa ngozi kutoka kata ya Muungano  amesema mafunzo ya jinsi ya kutumia na kurejesha mkopo kutoka halmashauri yamewasaidia kuwa na uelewa na watayafanyia kazi katika kupata faida kubwa na kurejesha mkopo huo.

Aidha Vikundi saba vya wanawake, kimoja cha watu wenye ulemavu na vikundi vitatu vya vijana vimenufaika na mkopo huo wa shilingi 25,600,000 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Hai ili kuwaongezea wananchi husika uwezo wa kujiongezea kipato na kureshesha fedha hizo bila riba ili ziweze kuwasaidia wengine kuinuka kiuchumi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Ujenzi Wa Bweni La Shule Ya Machame Kukamilika Kabla Ya June 19

    May 29, 2025
  • Vijana Wasauriwa Kutumia Fursa

    May 27, 2025
  • Wafanyabiashara Wa St Stend Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Wafanyabiashara Wa Send Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai