• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mkopo Wa Shilingi Milioni 142 Watolewa Kwa Vikundi Vya Wanawake Vijana Na Watu Wenye Ulemavi

Imetumwa: February 8th, 2023


Mbunge wa jimbo la Hai Saashisha Mafuwe amekabidhi mikopo inayotokana na asilimia 10 ya makusanyo ya halmashauri ya wilaya ya Hai yenye jumla ya shilingi Milioni 142 katika vikundi vya Vijana,  wanawake na watu wenye ulemavu

Akikabidhi  mikopo hiyo kwa vikundi vya vijana,  wanawake na watu wenye ulemavu Mbunge wa jimbo la Hai Saashisha Mafuwe amewataka wale wote waliopata mikopo kuzalisha ajira zaidi miongoni mwa wanakikundi na jamii kwa ujumla kama ilivyo adhima ya serikali.

Amesema kuwa vikundi hivyo ni vyema vikatambua kuwa  fedha hizo si zawadi bali ni mkopo ulio na masharti nafuu kwa lengo la kusaidia jamii kujikwamua kiuchumi.


"Ndugu zangu mnaopokea mikopo hii kila mara nasema mikopo hii sii zawadi bali ina masharti nafuu na hivyo tunapaswa kuzirejesha,  na hapa naomba niwaambie hatutomfumbia macho ambaye hatafanya rejesho kwakuwa tukirejesha tunatoa fursa kwa vikundi vingine kuzidi kukopesheka". Alisema Saashisha Mafuwe.

Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya Hai juu ya suala la utoaji wa mikopo hiyo,  Mkuu wa wilaya ya Hai Amir Mkalipa amewaomba madiwani wa halmashauri hiyo kushirikiana na serikali katika kuhakikisha vikundi vinavyopata mikopo vinarejesha kwa wakati kwani madiwani hao ndio wanashiriki kwa hatua za awali za kuviidhinisha vikundi hivyo ili kupewa mikopo hiyo.


Mkalipa  amesema  kuwa mbali na jitihada zinazofanywa na madiwani,  ofisi ya mkurugenzi na serikali kwa ujumla katika utoaji wa mikopo ni vyema kutambua kuwa kila mmoja anawajibu wa kuhakikisha fedha hizo za vikundi zinarejeshwa kwa wakati.


"Naombeni wote tutambue kuwa swala la vikundi kufanya marejesho kwa wakati ni ajenda yetu sote hapa ndani,  sii agenda ya mkurugenzi pekee wala mbunge wala diwani ni ya kila mmoja wetu na mimi kama mkuu wa wilaya nitashirikiana nanyi nyote kuhakikisha vikundi hivi vinarejesha fedha hizo kwa wakati" Alisema Mkalipa.


Akizungumza katika makabidhiano hayo,Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Mhe Edmund Rutaraka amewapongeza madiwani na wataalamu wa halmashauri kwa kusimamia vema na kuhakikisha upatikanaji wa fedha hizo za mikopo.

“Pesa hizi tunazo enda kutoa ni zao  halmashauri ya wilaya ya Hai,maanake  ni kwamba inatokana na asilimia kumi ya mapato yale ya ndani ambayo tumetenga kwa ajili ya vikundi vyetu vya akina mama,vijana na watu wenye ulemavu”

Awali akisoma taarifa ya utoaji wa mikopo kwa vikundi hivyo,  mkuu wa divisheni ya maendeleo ya jamii Robert Mwanga amesema kuwa jumla ya shilingi milioni 142 zimetolewa hii leo kwa vikundi  7 vya wanawake,  vikundi 4 vya vijana na walemavu 3 ikiwa ni asilimia 10 ya makusanyo ya halmashauri ya wilaya ya Hai.


Miongoni mwa vifaa vilivuokabidhiwa kwa vikundi hivyo ni pamoja na pikipiki za magurudumu matatu (Guta),  pikipiki za magurudumu mawili kwaajili ya kubebea abiria huku vikundi vingine vikiwa na miradi mingine kama vile usindikaji wa ndizi na parachichi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai