• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

MKUREGENZI HAI APONGEZA IDARA YA AFYA

Imetumwa: August 10th, 2018

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashari ya Wilaya ya Hai ameipongeza Idara ya Afya kwa kusimamia vema watoa huduma katika Wilaya hiyo hali iliyosababisha Wilaya kufanya vizuri katika tathmini ya ubora wa huduma inayofanywa na  wizara ya afya kupitia mpango wa  matokeao makubwa sasa iliyofanywa na Wizara ya Afya  kwa mwaka huu  ambapo Wilaya ya Hai imepata alama sitini na mbilii (62)  na kushika nafasi ya pili Kimkoa ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2016 iliyokuwa na alama tano  (5).

Amesema mabadiliko hayo yamewekezana kutokana na usimamizi dhabiti na ushirikiano ulipo kati ya Idara hiyo na vituo vyote vya Afya kwa kuwa tathimini hiyo ufanywa kwenye vituo na hosptali zote za  binafsi, taasisi za dini na za serikali  na kuitaka Idara hiyo kuendelea kusimamia vituo hivyo ikiwa ni pamoja na kuwapa miongozo mbali mbali ya Serikali kwa wakati inapotokea mabadiliko.

Mkurugenzi ametoa pongezi hizo wakati wa kikao cha kuiaga bodi ya Afya Wilaya kilichofanyika jana ambapo pia ameitaka  idara hiyo kuweka mkakati wa kutoa elimu kwa jamii  juu ya lishe na  mfumo wa ulaji bora  kwa jamii kupitia vyombo vya habari  na mikutano mbali mbali ya kijamii ili  kuboresha afya za wananchi na kuipunguzia serikali gharama  inayotumika kugharamia magonjwa ambayo yanasababishwa mfumo mbovu wa leshe na wananchi kutofanya mazoezi.

‘Ni kweli tumetoka asilimia tano kwenda asilimi sitini na mbili,tusiishie hapa tuendelee kufanyia kazi maeneo ambayo yamekuwa na changamoto zilizojitokeza  ili kwenye tathimini inayofuta tufanye vizuri zaidi, kwa vile vituo kumi bora  vya wilaya vipewe vyeti na Wilaya hii ni motisha kwa vituo hivi vilivyofanya vizuri na itaamusha hari kwa vile vituo ambavyo havikufanya vizuri kwa kipindi hiki ,lakini pia tuweke bidii na uwajibikaji zaidi kwa dhamana kubwa ya kuokoa maisha ya wananchi wetu.’alisisitiza Sintoo.

Akisoma taarifa ya matokeo ya tathimini ya Ubora, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Hai dkt Irine Haule alisema matokeo hayo yamepatikana baada ya kupitia vituo vyote 61 vya kutolea huduma vilivyopo wilayani hai, na kwamba tayari wameweka mikakati ya kutatua baadhi ya changamoto zilizojitokeza ikiwa ni pamoja na uchakavu wa miundo mbinu,uhaba wa wataalam wa maabara,kukosekana na dawa muhimu ya dharura na kukosa miundo mbinu ya watu wenye ulemavu na kwamba tayari baadhi ya changamoto hizo zitafanyiwa kazi kupitia utekelezaji wa bajeti  2018/2019.

Dkt Haule  amewashukuru wadau na wajumbe wa bodi ya afya kiwilaya  kwa jitihada zao katika kuboresha na kusaidia mafanikio kupatikana na kuahidi kushirikiana na wadau wote hasa wamiliki wa vituo vya afya vya taasisi za dini na binafsi ili kuendelea kufanya kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti  wa bodi aliyemaliza muda wake ndugu Invocativith Swai amesema bodi hiyo inayomaliza muda wake imeweza kusimamia ukarabati wa vituo vitatu vya afya ,kuanzishwa kwa duka la dawa katika hospitali ya wilaya ,ukamilishaji wa wodi ya wananwake pamoja na kuhakikisha upatikanajia wa vifaa tiba, dawa na vitendanishi katika vituo vyote vya kutolewa huduma kwa asilimia Zaidi ya 80  na ununuzi wa jenereta hali ambayo imesadia kuboresha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.

Naye dkt Grace kutoka Moshi Specialist akielezea siri ya mafanikio ya kituo hicho kuwa kushika nafasia ya kwanza kiwilaya na nafasi ya pili kimkoa ni ushirikiano na umoja katika utekelezaji wa majukumu yao ikiwa ni pamoja na ushirikiano mkubwa kutoka kwenye uongozi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Hai kutokana na usimamizi na ukaguzi wa mara kwa mara uliofanywa na timu ya wataalam kutoka Idara ya afya.

Katika matokeo hayo Halmashauri ya Hai imefanikiwa kutoa vituo vya Afya vitatu ambavyo vimafanikiwa kuingia kwenye kumi bora Kimkoa ,vituo hivyo ni Hospitali ya Wilaya ya Hai,kituo cha Afya cha Kisiki pamoja na Moshi Specialist.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai