• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mkurugenzi Awataka Wananchi Kchangamkia Fursa za Mikopo ya Halmashauri

Imetumwa: February 28th, 2020

Jamii katika Wilaya ya Hai imetakiwa kuchangamkia fursa za mikopo inayotolewa na Serikali kupitia halmashauri ili kujitengenezea mazingira ya kujiimarisha kiuchumi na kuboresha hali ya maisha kwenye kaya na hatimaye taifa zima.

Akizungumza wakati wa kukabidhi fedha za mkopo kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo amesema kuwa mikopo hiyo inatolewa kwa mujibu wa sheria na kwamba halmashauri yake itahakikisha mikopo inatolewa kwa wahusika.

Akikabidhi shilingi milioni 53 kwa vikundi 11 kati yao vikundi vya wanawake 5 vimepewa shilingi 21,400,000 vikundi vya vijana 4 vimepewa shilingi 21,402,028 na vikundi 2 vya watu wenye ulemavu wamepatiwa shilingi 10,700,876; Sintoo amesema ni wajibu wa kila kikundi kureshesha fedha walizokopa ili ziweze kukopeshwa kwa vikundi vingine.

“Kila kikundi kinachoomba mkopo kitapatiwa; cha msingi wawe wamekidhi vigezo na matakwa ya kufaidika na mkopo huu.” Amesema Sintoo.

“Maafisa Maendeleo ya Jamii; muwaelimishe wananchi taratibu za kuomba mkopo lakini pia wale wanaokosa muwaambie sababu za wao kukosa mkopo ili kuondoa manung’uniko miongoni mwa jamii kwani kupata mkopo hakuzingatii aina yoyote ya upendeleo” Ameongeza.

Kwa upande mwingine Katibu Tawala Wilaya ya Hai Upendo Wella ameviasa vikundi vilivyopatiwa mkopo kutumia fedha hizo kutekeleza malengo waliyojiwekea hususani yale waliyotengenezea andiko lililofanya wapate mkopo huku akiwakumbusha kuzingatia mafunzo waliyopewa na wataalamu.

Wella amesema lengo la mkpo huo ni kuwainua wananchi kiuchumi hivyo matumizi sahihi ya fedha hizo yatachangia kutimia kwa lengo hilo la serikali inayofanya juhudi za kuelekea uchumi wa kati.

Naye Johnson Mushi mwenyekiti wa kikundi cha Mkombozi Albino walionufaika na mkopo huo kwa mara ya pili amesema kuwa walipewa mkopo mwaka juzi walioutumia kwenye kilimo cha viazi ambapo walipata faida na kuweza kureshesha mkopo vizuri na sasa wameomba tena ili kuongeza uzalishaji kwenye kilimo cha viazi na kuwashauri waombaji wengine kutumia fedha hizo kwa uaminifu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai