• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mkurugenzi Halmashauri ya Hai Awakumbusha Watumishi Maadili Kazini

Imetumwa: October 5th, 2020

Watumishi wa Umma wametakiwa kutekeleza majukumu waliyonayo kwa wananchi kwa kufanya kazi kwa bidi na kuzingatia sheria na taratibu za kazi.

Akiongea kwenye kikao cha kawaida cha watumishi; Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Yohana Sintoo amesema ni heshima kuajiriwa na Serikali hivyo watumishi wanatakiwa kufanya majukumu yao kwa uaminifu.

“Sisi tumebahatika kupata kazi; tujitahidi kile kidogo tunachopata tuhakikishe kinatumika  kwenye matumizi sahihi” Amesema Sintoo.

Sintoo amewakumbusha watumishi kuhusu utaratibu wa watumishi kutoka nje ya eneo la kazi ikiwemo kusafiri kwenye wilaya na mikoa mingine.

Aidha, Sintoo amewataka watumishi kutumia ujuzi wa wataalamu wengine waliopo kwenye halmashauri katika kusaidiana katika shughuli za kujiongezea kipato kama kilimo na ufugaji ili kuwafanya watumishi wa umma kuishi maisha mazuri na familia zao.

Kwa upande wake Afisa Utumishi Augustina Kimbache ameelezea utaratibu unaowataka watumishi kujaza fomu za ruhusa wanapohitaji kwenda nje ya eneo la wilaya wanakofanyia kazi ili kuweka kumbukumbu na kfahamika mahali walipo.

“Utaratibu wa kuomba ruhusa unawahusu watumishi wote pamoja na wale wanaofanya kazi kwa mkataba wa muda maalumu kama kujitolea na wanafunzi wa mazoezi ambao wanafanya kazi chini ya Mkurugenzi Mtendaji” Ameongeza Kimbache.

Kwa upande mwingine Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Mwl. Julius Mduma amewasilisha shukrani za idara yake kwa Mkurugenzi Mtendaji kwa namna alivyoendesha harambee maalumu ya kuboresha miundombinu ya shule ya Sekondari Mailisita.

Mduma amesema kuwa kiasi cha Shilingi milioni 65 zimepatikana kupitia michango ya wadau kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vyumba vya maabara pamoja na vyumba viwili vya madarasa kwenye shule hiyo.

Katika harambee hiyo Mkurugenzi Mtendaji ameahidi kujenga chumba kimoja cha darasa na samani zake vikiwa kwa ujumla na thamani ya shilingi milioni 25 ikiwa ni mchango wa halmashauri katika kuimarisha sekta ya elimu katika Wilaya hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai ameweka utaratibu wa kukutana na watumishi wa idara na vitengo vyote wanaofanya kazi makao makuu ya halmashauri hiyo kila siku ya Jumatatu ili kufanya tathmini ya wiki iliyokwisha na kuweka mikakati ya utekelezaji wa kazi kwa wiki inayoanza.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai