• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mkuu wa Mkoa Asuluhisha Polisi na Wananchi wa Kia

Imetumwa: April 24th, 2019

MKUU wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira, ameagiza kuchukuliwa hatua za kisheria askari polisi wa kituo cha polisi cha Kia wilaya Hai wanaotuhumiwa kuwabugudhi wananchi wanaozunguka kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Kilimanjaro (KIA)

Dkt. Mghwira amemwagiza kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro kuchunguza tuhuma za askari wa kituo hicho kufyatua risasi hewani kwenye makazi ya watu pamoja na kuwakimbiza watoto wa wafugaji waliokuwa katika malisho ya mifugo.

Aidha ameagiza kufanyike uchunguzi juu ya mkuu wa kituo cha Kia wa kwa nini hakuchukua hatua kwa askari wa kituo chake wanaotuhumiwa kwa utovu wa nidhamu kutokana na tukio lililotokea Aprili 7 mwaka huu.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sanya Stationi katika mkutano wa hadhara, Dkt Mghwira, amemtaka Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro RPC Hamis Issa kuchunguza utendaji wa askari wa kituo hicho ambao umekuwa ukilalamikiwa na wanachi wa maeneo hayo.

Amesema tukio la askari hao kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani na kuwabugudhi wananchi linaleta taswira hasi kwamba serikali ndiyo inakandamiza wananchi wake na kususutiza umuhimu wa kudumisha amani na maelewano baina ya jamii zinazopakana kwenye eneo hilo.

“Askari tunawaheshimu sana; lakini pia ni sura ya serikali, sasa ikitokea askari amepiga mwananchi inaonekana kama serikali ndio imepiga mwananchi; hili naomba liangaliwe na lidhibitiwe vizuri” amesema Mghwira.

“Mimi sijamtuma mtu yeyote kuhusiana na suala lolote kuhusu KADCO hivi karibuni, na kama kuna anayesema nimemtuma, kama ni askari, Kamanda wa Polisi shughulika naye.”

Amesema kuwa serikali inatambua kuwa kuwa eneo hilo licha ya kuwa na uwanja wa ndege wa kimataifa pia wapo watu wanaoishi katika maeneo hayo na lazima waishi  kwa amani wakati mgogoro wa msingi ukiendelea kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Amesema kuwa tatizo hilo pia linasababishwa na kutokuwepo kwa miundombinu ya kulishia mifugo na kutokwepo na mipaka imara itakayosaidia kuimarisha hali ya ulinzi kwenye maeneo yote na kuepusha migogoro hiyo.

Akizungumzia tukio hilo kijana Samweli Lazaro amesema siku ya tukio alikamtwa na askari na kukalishwa chini na kunyang’anywa silaha za jadi ambazo alikuwa nazo machungani.

“Walinikalisha chini na kunishikia bunduki na kuninyang’anya viatu na kuwafukuza watoto mpaka nyumbani na kupiga risasi mbili hewani” amesema.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kia Yohana Laizer amesema kuwa tatizo kusumbuliwa na askari wa kituo cha KIA limekuwa sugu na limekuwa likitokea mara kwa mara na wakati mwingine hukamata mifugo  na kuifungia kituoni.

“Tumechoka kufukuzwa na polisi kama wakimbizi, watoto wa shule wamekuwa wakikimbizwa na mbuzi zimekuwa zikifungiwa mahabusu kama watu, naomba utusaidie kuhusu suala hilo”amesema Diwani Laizer.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya amemweleza Mkuu wa Mkoa kuwa kuna hali ya kutoelewana kati ya wananchi wanaozunguka maeneo ya uwanja huo na kukiri kupokea malalamiko ya wananchi hao wakidai kunyanyaswa na polisi wa Kia.

“Mgogoro uliopo hapa ni ule wa KADCO na wananchi na polisi wamekuwa wakitumia nguvu kubwa kwa wananchi lakini hakuna kiongozi wa serikali aliyetuma kunyanyasa wananchi ”amesema Ole Sabaya

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro (RPC)Hamisi Issa amesema askari waliohusika na tukio hilo watachukuliwa hatua za kisheria wakibainika kufanya jambo hilo ambalo ni kinyume na taratibu za jeshi.

Aidha RPC Issa amewataka askari polisi katika mkoa wa Kilimanjaro kushirikiana kwa karibu na viongozi wa kijamii waliochaguliwa na wananchi ili kuimarisha mahusiano mazuri na kuimarisha ufanisi wa kazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai