• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mkuu Wa Mkoa Kilimanjaro Aridhishwa Na Ujenzi Wa Madarasa Wilaya Ya Hai

Imetumwa: December 13th, 2022

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu ameipongeza wilaya ya Hai kwa kukamilsha ujenzi wa madarasa 10 ya sekondari ndani ya muda uliopangwa na kwa ubora  huku akizitaka halmashauri zingine kujifunza Hai.

Akizungumza katika makabidhiano ya madarasa hayo yaliyofanyika leo Disemba 13, 2022 katika Shule ya Sekondari Hai,  Babu ameipongeza halmashauri hiyo kwakutumia kiasi  cha fedha kilichotolewa na serikali kwa kujenga madarasa yenye viwango sahihi yapatayo 10 na ofisi za waalimu katikati.

Pia Mkuu huyo wa Mkoa ametoa maagizo kwa halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa mwezi januari wanafunzi wote wanaotakiwa kuendelea na masomo wanafanya hivyo mara moja kwani serikali imejenga madarasa hayo kwaajili ya wanafunzi hao na kinyume na hapo serikali itachukua hatua kali kwa wale wote watakao kwamisha wanafunzi kujiunga na masomo mwakani.

Aidha ameagiza Halmashauri hiyo ya Hai na halmashauri zingine katika mkoa wa Kilimanjaro kutumia fedha za ndani za Halmashauri kukarabati madarasa chakavu huku akiwapongeza wananchi waliojitolea michangango yao mbalimbali ili kununua marumaru kwa ajilia kuongeza ubora wa majengo hayo.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mkuu wa wilaya ya Hai Juma Irando amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za ujenzi wa madarasa katika wilaya ya Hai jambo ambalo limetatua tatizo la pungufu wa madarasa na kwamba wanafunzi wote watakaochagulia kujiunga na elimu ya sekondari katika wilaya ya Hai hawatakosa nafasi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai, Edmund Rutaraka amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta fedha nyingi za mradi katika wilaya ya Hai, hasa katika sekta ya Afya, barabara, Maji na elimu.

“Hii shule ina bahati  kuanzia mwaka  2020  hadi sasa tumejenga madarasa 11, tulianza na madarasa mawili, tukajenga madarasa sita na sasa tumejenga madarasa matatu  kwa hiyo tunaweza kusema tuna shule ndani ya shule”amesisitiza Rutaraka

Naye mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Hai Wang’uba Maganda amesema serikali  imeamua kuwekeza kwenye mambo ya maendeleo hasa huduma muhimu za kijamii na muda si mrefu changamoto nyingi za kijamii zitakuwa zimetatuliwa.

“Tunamshukuru sana mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Samia Suluhu  Hassan kwa kujali sana suala la kijamii hasa elimu, maji na barabara, watu wa Hai tunashukuru sana na tunazidi kumuombea kwa Mungu”amesema Maganda

Awali akisoma taarifa ya ujenzi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Hai Juma Irando, Mkuu wa divisheni ya Elimu Sekondari Julius Mduma amesema wilaya ya Hai ilipokea milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 10 katika shule za Rundugai darasa moja, Hai madarasa matatu, Mukwasa darasa Moja, Neema darasa moja, Tumo darasa moja, Longoi madarasa mawili, na Roo darasa moja.Ujenzi wa madarasa yote umekamilka tayari kwa kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza Januri 2023.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai