• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Mkuu wa Wilaya ya Hai Kujenga Ukumbi Kituo cha Polisi Bomang'ombe

Imetumwa: April 15th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ametangaza nia ya kujenga ukumbi wa mikutano kwa ajili ya matumizi ya jeshi la polisi wilayani humo.

Akizungumza mbele ya maafisa na askari katika viwanja vya polisi wilayani Hai Ole Sabaya amesema anachangia shilingi million tatu za kukarabati  gari la polisi na kwamba kiasi cha shilingi million ishirini kitapatikana kwa ajili ya kujenga ukumbi wa mikutano.

Akikabidhi fedha taslimu kiasi cha shilingi million tatu za kuchangia kufanyia marekebisho gari la polisi kwa ajili ya matumizi ya jeshi hilo; Ole Sabaya amesema ofisi yake na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wataendelea kutatua changamoto zinazojitokeza ili kurahisisha utendaji wa jeshi hilo.

“Nakabidhi fedha hizi ili ziwasaidie kutatua changamoto yenu ya gari na mtambue kwamba serikali ipo pamoja nanyi na itashirikiana na jeshi kutatua changamoto zitakazojitokeza” amebainisha Ole Sabaya.

Aidha Ole Sabaya amewataka maafisa na askari polisi wa wilaya ya Hai kufanya kazi zao kwa weledi na kuwahudumia wananchi kwa kuzingatia sheria na taratibu za kazi yao ili kuepuka malalamiko.

Awali akimkaribisha Mgeni rasmi, Katibu Tawala wilaya ya Hai Upendo Wella amewakumbusha maafisa na askari pamoja na watumishi wote wa umma katika wilaya ya Hai kufanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia miongozo ya kazi zao.

“Naendelea kusisitiza kwamba tuendelee kufanya kazi zetu kwa kuzingatia nidhamu na sheria zinazotuongoza kuhakikisha kuwa tunawatumikia wananchi kwa haki na usawa ili kutekeleza malengo makuu ya kuwahudumia vizuri wananchi wa wilaya ya Hai”. Amesema Wella.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo amepongeza ushirikiano uliopo kati ya jeshi la polisi na ofisi yake kwa kufanya kazi pamoja na kwa karibu kwenye mambo yanayowakutanisha na kuomba ushirikiano huo kuendelezwa kwa manufaa ya wananchi wa wilaya ya Hai.

Ole Sabaya ametumia hadhara hiyo kumtambulisha Brighton Mushi mdau wa maendeleo atakayeshirikiana naye kufanikisha azma ya kujenga ukumbi ambaye ni mwenyeji wa wilaya ya Hai anayefanya shughuli zake mkoani Arusha.

Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Ole Sabaya amekuwa mstari wa mbele kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa umma katika wilaya yake kwa kuchangia miradi mbalimbali inayoibuliwa na wananchi pamoja na kununua pikipiki tatu na kukarabati nyingine tatu kwa jaili ya matumizi ya jeshi la polisi wilayani humo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai