• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Naibu Waziri Mabula Awageukia Wanaodaiwa Kodi ya Ardhi

Imetumwa: February 28th, 2018

Naibu Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Anjelina Mabula ameitaka idara ya ardhi Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, kutowafumbia macho wadaiwa sugu waliogoma au kuchelewa kulipia kodi ya ardhi wanazomiliki.

Ametoa wito huo wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua mpaka wa Tanzania na Kenya katika mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Arusha na Mara pamoja na kukagua mfumo wa ulipaji wa kodi ya ardhi katika halmashauri ili kuongeza kiwango cha ulipaji wa kodi.

Mabula amesema kuwa kumekuwepo na  changamoto ya watu kumiliki viwanja huku wakikataa kuvipima na kuchukua hati  jambo linaloleta migogoro mingi katika maeneo yao huku serikali ikipoteza kodi ya ardhi hivyo ni vema  kufika mwisho wa kuwavumilia.

Mabula ameongeza kuwa Wizara ya ardhi inapoelekea katika bajeti itaenda  kubadilisha baadhi ya taratibu ili kuweza kuvitambua viwanja ambavyo havijapimwa ili kubadilisha sheria na kuweka sheria itakayo mbana mmiliki kulipa na kuepuka wananchi kuibia serikali kodi, na kuondoa changamoto hiyo.

Aidha amesema kuwa wizara imejaribu kutoa vitendea kazi vitakavyosaidia kutunza kumbukumbu, kutambua wadaiwa na njia ya wao kufanya kazi kwa ufanisi, hivyo asingependa kusikia kuwa vitendea kazi hivyo vimeshindwa kufanyakazi kwa kutegemea wizara kukarabati au kuleta vipya, jambo ambalo ni kinyume kwani halmashauri ndio inayotakiwa kuendelea kuhudumia vifaa hivyo kwa kutenga fungu.

Awali akisoma ripoti ya utekelezaji wa ukusanyaji wa kodi ya ardhi kwa njia ya mfumo wa kisasa uliowekwa na Wizara; Kaimu Mkuu wa Idara ya ardhi Jacob Muhumba ametaja changamoto zilizopo za utumizi wa mfumo huo kufanyakazi taratibu sana kutokana na tatizo la mtandao.

Katika kutatua changamoto hiyo wamelazimika kutoa taarifa kwa katibu mkuu wizara ya ardhi hivyo kuamini kuwa changamoto hiyo itatatulika na kuendelea kutoa huduma hiyo kama ilivyokusudiwa.

Katika kuzungumzia migogoro ya ardhi ndani ya Wilaya ya Hai Jacob amesema kuwa migogoro ni ya kawaida huku mgogoro mkubwa ukiwa ni wa wananchi wa vijiji vya sanya station, Tindigani na Chemka kutokana na baadhi ya kaya katika vijiji hivyo kuingia katika eneo la uwanja wa Ndege jambo ambalo bado linashughulikiwa na ofisi ya waziri Mkuu pamoja na TAMISEMI.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Ujenzi Wa Bweni La Shule Ya Machame Kukamilika Kabla Ya June 19

    May 29, 2025
  • Vijana Wasauriwa Kutumia Fursa

    May 27, 2025
  • Wafanyabiashara Wa St Stend Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Wafanyabiashara Wa Send Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai