• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Ofisi ya Waziri Mkuu Yawafuta Machozi Wahanga wa Mafuriko Wilaya ya Hai

Imetumwa: May 9th, 2021


Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha kushughulikia maafa imetoa msaada wa vifaa kwa kaya zilizokumbwa na mafuriko katika kata za Weruweru, Masama Mashariki na Machame Magharibi wilaya ya Hai kutokana na mvua zilizosababisha mafuriko kati ya tarehe 21 na 22 mwezi April.


Msaada huo uliotolewa umehusisha vifaa kama magodoro 250, mablanketi 83, ndoo ndogo 167, sufuria 167, madumu ya maji 250, mikeka 1,666 na ndoo kubwa 67 ambavyo vitagawiwa kwa wahanga wa mafuriko katika Wilaya ya Hai.


Pamoja na msaada huo; wahanga hao wamepokea msaada mwingine kutoka Wizara ya Kilimo kupitia Wakala wa Hifadhi ya Chakula Kanda ya Kaskazini Arusha ambayo imetoa tani 33 za mahindi kugawiwa kwa wahanga hao.


Akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya Serikali, Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ametoa pole kwa wananchi waliofikiwa na maafa hayo huku pia akiishukuru Serikali kuu kwa msaada walioutoa.


Sabaya ametumia shughuli hiyo kutambua mchango wa wawakilishi wa wananchi akiwemo Mbunge wa Jimbo la Hai Saashisha Mafuwe pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai na Diwani wa Kata ya Muungano Edmund Rutaraka kwa juhudi walizoonesha kuwatembelea wahanga na kushirikiana nao.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo amesema kwa sasa ofisi yake inaliratibu zoezi hilo kwa ukaribu na hadi kufikia mwishoni mwa wiki ijayo vifaa vilivyotolewa vitakuwa tayari vimewafikia walengwa.


Awali akisoma taarifa ya maafa mbele ya Mkuu wa wilaya ya Hai, Afisa Mazao Wilaya ya Hai Zefania Gunda kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo amesema kuwa kaya zilizokumbwa na mafuriko ni 543 na baada ya kufanyiwa tathimini imebainika kuwa zinazohitaji msaada wa dharura ni kaya 253 na 13 zikiachwa bila makazi baada ya kutokea kwa maafa hayo.


Maafa hayo yamesababishwa na mvua zilizonyesha ukanda wa juu wa Wilaya ya Hai usiku wa tarehe 21 kuamkia 22 mwezi Mei yaliyopelekea maporomoko ya maji yenye kasi kubwa na kusababisha madhara kwenye kata 10 za wilaya hiyo huku athari zaidi zikionekana kwenye kata za Weruweru, Masama Mashariki na Machame Magharibi.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai