• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Serikali Wilaya ya Hai Yatengua Sheria ya Kijiji ya Katazo la Kutembea Usiku

Imetumwa: July 3rd, 2020

Serikali katika Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro imetengua katazo la wananchi kutembea usiku katika Kijiji cha Isuki, Kata ya Masama Kati na kuagiza kupelekwa askari wa jeshi la polisi na jeshi la akiba kuimarisha ulinzi wa watu na mali zao.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara kwenye Kijiji hicho Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya amesema kuwa katazo la muda wa wananchi kutembea linatolewa kwa mamlaka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pekee.

“kwani ninyi mnaishi kwenye nchi yenu peke yenu? Niwaambie kwamba hakuna Jamhuri ya Isuki, na maamuzi ya kuzuia watu kutembea usiku nio jukumu la kijiji; hata mimi mkuu wa wilaya na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hatuwezi kutoa maamuzi hayo” amesema Sabaya.

Sabaya amesitisha shughuli zote za sungusungu wa kijiji hicho ambao kwa maelekezo ya Mwenyekiti wa Kijiji Rabikira Makere wamekuwa wakiwakamata na kuwaadhibu wananchi walioonekana kutembea Zaidi ya saa mbili usiku na nafasi yao kuchukuliwa na askari wa jeshi la akiba.

Aidha Sabaya ameagiza TAKUKURU Wilaya ya Hai kuanzisha uchunguzi wa matumizi mabaya ya madaraka kwa mwenyekiti wa kijiji hicho pamoja na baadhi ya wasaidizi wake wanaotuhumiwa kuhusika na unyanyasaji kwa wananchi.

Wakizungumza kwenye mkutano huo wakielezea madhila waliyopitia wakati wa kutekelezwa kwa katazo hilo baadhi ya wananchi wamesema kuwa wamekuwa wakikamatwa na sungusungu wa kijiji huku wakiadhibiwa kwa fimbo na faini ya mali au fedha taslimu.

Neeman Makere  ni mmoja wa wanachi waliowahi kukutana na mkono wa sheria hiyo ya kijiji iliyotekelezwa kwake baada ya kutembea Zaidi ya muda ulioelekezwa na uongozi wa kijiji chao.

“Nilitoka kwa baba yangu wakanikamata wakaniingiza ndani ya ofisi nilipohoji kuhusu kosa langu na kutaka wanipeleke kituo cha polisi Bomang’ombe; mwenyekiti akawaambia wanitoe wanipeleke ‘goligota’ ndipo wakanitoa nje wakanifunga na pingu kwenye nguzo wakanichapa viboko 60 wakachukua elfu 30 na simu yenye thamani ya shilingi elfu 25”. Ameeleza Makere.

Naye Mtendaji wa Kijiji hicho Jared Swai amesema kuwa katika muhtasari wa vikao vya halmashauri ya kijiji hawakukubaliana uwepo wa sheria hiyo na ameshangazwa na adhabu zinazotolewa kwa wananchi hao bila utaratibu na kukiri kupokea malalamiko kutoka mwanchi ambae alikutana na tatizo hilo.

Swai amesema mbele ya Mkuu wa Wilaya kuwa amekuwa na wakati mgumu kutekeleza majukumu yake kutokana na tabia ya Mwenyekiti wa Kijiji kuhodhi madaraka na wakati mwingine kuingilia utendaji wa serikali kwa Imani kuwa yeye (mwenyekiti) ndiye sauti ya mwisho ya maamuzi kwenye kijiji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji hicho Rabikira Makere amesema kuwa adhabu hiyo ilipitishwa kwenye mkutano wa kijiji ikiwa ni jitihada za kukabiliana na matukio ya uhalifu ikiwemo wizi, ukabaji na hata matukio ya watu kuvamiwa na kuuawa yaliyokithiri kwenye kijiji chao.

Mkuu wa Wilaya amechukua maamuzi kuingilia mgogoro huo baada ya kupokea malalamiko ya wananchi waliokuwa wakikandamizwa na sheria hiyo iliyowataka kutotembea zaidi ya saa mbili usiku na kwamba waliokamatwa waliadhibiwa kwa kufungwa pingu, kuchapwa fimbo 60, kulipa faini ya fedha kuanzia Sh. 30,000 hadi Sh. 80,000 au kupakwa upupu ‘washawasha’.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai