• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Serikali Wilayani Hai Kuhakikisha Wanafunzi Wanapata Chakula Shuleni

Imetumwa: January 23rd, 2020

Serikali katika Wilaya ya Hai imeazimia kusimamia upatikanaji wa chakula kwa wanafunzi wote wanaosoma katika shule za wilaya hiyo.

Msimamo huo wa serikali umetolewa mapema leo na Mkuu wa Wilaya ya Hai ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya alipofanya kikao na Wakuu wa Shule za Msingi kilichohudhuriwa pia na Wenyeviti wa Kamati za shule pamoja na wenyeviti wa vijiji zilipo shule hizo.

Sabaya amesema kuwa ni sharti wanafunzi wote wapatiwe chakula shuleni huku akiwasisitiza wazazi kuhakikisha kuwa wanawajibika kuchangia michango ya chakula na kwamba mzazi atakaeshindwa kufanya hivyo atachukuliwa hatua za kisheria.

Sabaya amewakumbusha walimu kusimamia majukumu yao ya kufundisha na kuhakikisha wanafunzi wanaoletewa wanapata elimu wanayostahili, huku akiwakumbusha kamati za shule kutekeleza wajibu wao huku akiwasisitiza wazazi kuendelea na majukumu yao ya kuwapatia watoto mahitaji muhimu ikiwemo chakula, mavazi na daftari.

“Rais Magufuli anatoa shilingi bilioni 23.86 kila mwaka kwa ajili ya kuhudumia elimu bure ambayo inatumika kulipa ada za wanafunzi, kuhudumia miundombinu, kuhudumia shughuli za utawala wa shule kwa kila mwanafunzi aliyeandikishwa kwenye shule husika ” Amesema Sabaya.

“Serikali inachofanya ni kuondoa zile gharama zinazofanya mwanafunzi kutokusoma kwa raha kwa kurudishwa nyumbani kwa ajili ya kwenda kuchukua michango inayohusiana na ukaaji wake shuleni ambayo ilikuwa ada, dharura, madawati na michango mingine iliyokuwepo”

Aidha Sabaya amezitaka kamati za shule na wenyeviti wa vijiji kuacha kuingilia majukumu ya kitaaluma yanayofanywa na ili kuwapa nafasi walimu kuwaandaa wanafunzi kwa namna inayotakiwa huku akihimiza umuhimu wa kuwa na mahusiano mazuri kati yao.

Nao walimu wakuu wa shule kwa umoja wao wamemuhakikishia mkuu wa wilaya kuwa wataendelea kufanya kazi kwa bidi kwa kuzingatia sheria na taratibu za elimu kuhakikisha kuwa wilaya ya Hai inaendelea kufanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa ikiwemo Darasa la Saba na la Nne.

Kwa upande mwingine wenyeviti wa vijiji pamoja na wenyeviti wa kamati za shule wameahidi kutoa ushirikiano kwa walimu kwa kusimamia mambo yote yasiyohusu masuala ya taaluma ili kuwafanya walimu washughulikie malezi ya watoto kitaaluma na kuongeza ufaulu.

Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya akishirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya pamoja na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai wamejiwekea utaratibu wa kukutana na watumishi wa idara na vitengo vya halmashauri hiyo kila mwanzo wa mwaka kwa ajili ya kuweka mikakati ya utekelezaji wa kazi pamoja na kukutana mwisho wa mwaka kwa ajili ya kupima utekelezaji uliofanyika kitendo ambacho kimeongeza ufanisi wa watendaji kwenye halmashauri hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai