• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Serikali Yaipongeza Idara ya Afya Wilaya ya Hai Utoaji wa Chanjo

Imetumwa: November 15th, 2019

Serikali katika Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro imeipongeza Idara ya Afya wilayani humo kwa kuvuka lengo katika zoezi la utoaji wa chanjo ya Surua Rubela lililofanywa kwa Siku wiki moja na kufanikiwa kwa asilimia 114 ikiwa ni zaidi ya lengo lililowekwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Afya ya Msingi wilaya mapema leo Ijumaa katika kikao cha mrejesho wa Kampeni shirikishi ya chanjo ya Surua na Rubela kilichofanyika katika ukumbi wa hospitali ya wilaya ya Hai kikijumuisha wajumbe mbalimbali wa kampeni hiyo.

Awali akisoma taarifa ya kampeni hiyo Mratibu wa chanjo wilaya Michael Ndowa amesema kuwa mafanikio hayo yamechangiwa na msukumo na uhamasishaji wa viongozi wakuu wa wilaya wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya pamoja matangazo yaliyosambazwa kwa jamii kupitia Radio Boma Hai Fm ikitanguliwa na maandalizi ya kabla ya kampeni yaliyohusisha mafunzo kwa wasimamizi, wachanjaji na wahamasishaji.

Amesema kuwa mbali na asilimia hizo 114 kwa chanjo ya Surua na Rubela pia wamefanikiwa kutoa chanjo ya sindano ya Polio kwa asiilimia 107 na kupelekea wilaya ya Hai kuwa ya kwanza kwenye mkoa wa Kilimanjaro.

Kwa Upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Hai Dkt.Irine Haule amesema kuwa kampeni hiyo imekuwa na mafanikio makubwa kutokana na Halmashauri kutenga bajeti ya kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 10 ambayo iliungana na bajeti ya Wizara ya afya na kusaidia kuongeza idadi ya vituo vya kutolea huduma hiyo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo, amewataka watumishi wa umma katika Halmashauri yake kuendelea kuwa na ushirikiano katika utendaji wao wa kazi za kila siku za kuwahudumia wananchi ili kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli.

Zoezi la utoaji wa chanjo ya Surua, Rubela pamoja na Polio lilifanyika kote nchini October 17 hadi 22 mwaka huu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai