• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Serikali Yataka Ushirikiano wa NMB na halmashauri uimarishwe

Imetumwa: February 27th, 2020

Serikali katika Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro imepongeza ushirikiano uliopo kati ya benki ya NMB na mamlaka za serikali za mitaa hasa halmashauri ya wilaya ya Hai.

Akizungumza wakati wa kupokea msaada wenye thamani ya shilingi milioni 21 kutoka benki ya NMB; Mkuu (mshikizi) wa Wilaya ya Hai Agnes Hokororo amesema ushirikiano uliopo uendelee kuimarishwa ili kuwapatia wananchi huduma bora Zaidi.

“Niwaombe benki ya NMB, leo mmetusaidia kwenye maeneo ya afya na kilimo; niwaombe tuendelee kushirikiana kwenye maeneo haya mawili hasa kwenye zao la vanilla ambalo likipata huduma nzuri na wakulima wengi wakilima itasaidia kuongeza kipato cha wananchi ” Amesema Hokororo.

Aidha Hokororo amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya akishirikiana na Mganga Mkuu wa Wilaya kuhakikisha kuwa vifaa vilivyopokelewa vinafanya kazi iliyokusudiwa na vinasaidia kupunguza changamoto za wananchi.

Pia amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu wa Idara ya Kilimo wilayani Hai kutumia vizuri fedha walizopatiwa ili kuimarisha kilimo cha zao la vanilla huku akushauri uwezekano wa kuanzisha kitalu kitakachouza miche ya vanilla kwa halmashauri nyingine zinazofaa kulima zao hilo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo akizungumza wakati wa kupokea vifaa hivyo, ameishukuru benki ya NMB na kuahidi kutumia vizuri vifaa vilivyotolewa kwa ajili ya matumizi ya hospitali chini ya usimamizi wa Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Irene Haule lakini pia ameahidi kuzingatia matumizi sahihi ya fedha zilizotolewa kuimarisha kilimo cha vanilla Mkuu wa Idara ya Kilimo David Lekei.

Kwa upande wake Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini Aikansia Muro amesema benki ya NMB imejiwekea utaratibu wa kurudisha kwa jamii faida wanayoipata na kwa sasa wamijizatiti kumuunga mkono Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kusaidia shughuli za huduma ya jamii hasa elimu na afya huku akimhakikishia Mkuu wa Wilaya kuwa wataendelea kushirikiana na halmashauri ya Wilaya ya Hai kuboresha huduma kwa jamii.

Awali akisoma taarifa ya shughuli za kuimarisha zao hilo; Mratibu wa zao la Vanilla wilaya ya Hai Simon Gunda amesema kuwa fedha zilizotolewa na NMB zitatumika kuwafikia Zaidi ya wakulima 1,200 kwenye vijiji 43 katika kata 10 ambapo kila kijiji watachaguliwa wakulima 30 watakaopewa mafunzo ya zao hilo na watauziwa miche kwa bei ya ruzuku ambayo itanunuliwa kutokana na sehemu ya fedha iliyotolewa na benki ya NMB.

Benki ya NMB imetoa msaada wenye thamani ya shilingi miliani 21 kwa kutoa vitanda vinne vya kupumzikia wagonjwa na vitanda viwili kwa ajili ya kujifungulia lakini pia kutoa shilingi milioni 16 kwa ajili ya kuimarisha zao la vanilla.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai