• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Shirika la Nyumba la Taifa Lakamilisha Ujenzi Nyumba ya DC Hai

Imetumwa: May 26th, 2020

SHIRIKA la Nyumba nchini(NHC) limesema litaendelea kutekeleza miradi mbalimbali inayokabidhiwa na Serikali Kuu huku likizingatia viwango vinavyokubalika kitaalam.


Ahadi hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Dkt. Maulid Banyani, wakati wa hafla ya kukabidhi jengo jipya la ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, iliyofanyika wilayani humo mwishoni mwa wiki.


“Tunaishukuru Serikali, hususan ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwa kuendelea kuiamini NHC na kuipa miradi mbalimbali ambapo kwa sasa kuna miradi zaidi ya 40 ambayo inatekelezwa na NHC hapa nchini”, amesema.


Alisema NHC kuendelea kuaminiwa na Serikali na kupewa miradi hiyo ni kazi nzuri ambazo zimekuwa zikifanywa na shirika hilo wakati wa kutekeleza miradi mbalimbali ambapo alisema shirika hilo litaendelea kufanya kazi kwa weledi. .


Aidha amempongeza Rais Dkt.Magufuli kwa kuwa na maono yaliyopelekea Watanzania kuendelea kufanya kazi huku wakichukua tahadhari wakati Dunia ikiendelea kupambana na ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na virusi vya Corona.


“Kama tungelazimishwa kujifungia ndani kama mojawapo ya tahadhari ya kuepusha maambukizi mapya ya virusi vya Corona hata mradi huu usingeweza kukamilika kwa wakati uliowekwa na hapa ndipo umuhimu wa maono mazuri aliyokuwa nayo Rais wetu unapoonekana”, Ameongeza Dkt. Banyani.


Akitoa ripoti ya mradi huo,Yusuph Bigambo kutoka wakala wa Majengo Tanzania (TBA), taasisi hiyo ilisanifu na kusimamia mradi huo kama Mshauri Elekezi Mkuu kwa ushirikiano na Mshauri Elekezi Msaidizi upande wa Umeme na Mitambo.


“Mradi huu ambao umetekelezwa na NHC kama Mkandarasi Mkuu ulianza rasmi Mei, 2019 na kukamilika Mei, 2020; mpaka sasa umegharimu jumla ya shilingi 1,092,327,322.92”, alisema.


Akizungumza kwa niaba ya KatibuTawala Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Dkt. Hatib Kazungu, Katibu Tawala Msaidizi Sekretarieti ya Mkoa wa Kilimanjaro Bi Lyidia Riwa amelipongeza Shirika la Nyumba kwa kukamilisha mradi huo kwa muda na ubora uliotarajiwa.


“Nitoe rai kwa uongozi wa Serikali wilaya ya Hai kuhakikisha jengo hili linatunzwa vyema ili liweze kudumu kutokana na kuwa Serikali imetumia pesa nyingi katika kutekeleza mradi huu hii ikiwa ni sehemu ya ahadi ya Rais Dkt. Magufuli ya kuweko na ofisi bora nchini kote”, alisema.


Akitoa shukrani kwa niaba ya uongozi wa wilaya ya Hai, Katibu Tawala wa wilaya hiyo Upendo Wela, ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha zilizowezesha ujenzi wa jengo ambapo amesema miundombinu bora hiyo itakuwa chachu ya viongozi wa Serikali ya wilaya hiyo kuongeza ufanisi wa utendaji wake hasa katika kuwahudumia wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai