• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Silinde Azindua Huduma Afya ya Kinywa na Meno Wilayani Hai

Imetumwa: February 11th, 2021

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais –Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa David Silinde (MB) amewataka wananchi kuondoa hofu zinazosababishwa na taarifa za uongo zinazosambazwa dhidi ya ugonjwa wa Corona ila wachukue tahadhali za msingi zitakazoimarisha afya zao.

Ameyasema hayo leo Februari 11 wakati wa ufunguzi wa jengo la huduma za kinywa na meno katika hospitali ya wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro lililojengwa kutokana na fedha za makusanyo ya mapato ya ndani.

Ameitaka jamii kuzingatia maelekezo ya Serikali hasa yanayotolewa na Rais John Magufuli kuwa ugonjwa wa Corona unatibika kwa nguvu za Mwenyezi Mungu na kutumia dawa lishe kama inavyoshauriwa na wataalamu wa afya.

Aidha Naibu Waziri Silinde amezitaka halmashauri nyingine nchini kuiga mfano wa halmashauri ya Hai kwa kutekeleza miradi ya maendeleo yenye tija kwa wananchi kwa kutumia vyanzo vya fedha za mapato ya ndani badala ya kusubiri kila kitu kifanywe na serikali kuu.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ametumia uzinduzi huo kuwatoa hofu wananchi kuhusu  maambukizi ya ugonjwa wa Corona kwa kuwataka wasiogope kufanya shughuli zao za maendeleo kama ilivyo desturi na kujitafutia kipato chao na familia zao kwa kuwa hofu ndio inayokatisha maisha yao.

Amesema kumekuwepo dhana yenye mitazamo tofauti juu ya kila anayefariki dunia kuelezwa  kuwa amekufa kwa ugonjwa huo jambo hilo linasababisha wananchi kujawa na hofu na wengi wao kupoteza maisha na kusisitiza kuwa wilaya hiyo ipo salama.

Hata hivyo Sabaya amewataka wananchi kuendelea kuchukua hatua za kujikinga kwa kujifukiza majani yaliyoletwa na Mungu na kufanywa dawa ya kuwaponya na kuepuka matumizi ya chanjo ambayo ni biashara ya mabeberu na si salama sana.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa wilaya hiyo, Dkt Irene Haule amesema Jengo hilo la huduma za kinywa na meno limejengwa kwa gharama ya shilingi milioni 82 fedha ambazo zimetokana na mapato ya ndani.

Hata hivyo amesema kumekuwepo na changamoto ya upungufu kwa watumishi katika idara ya afya wilayani humo hasa katika kitengo cha huduma ya kinywa na meno kwani kati ya watumishi 10 wanaohitajika kwa sasa kuna watumishi watatu tu jambo ambalo linaleta changamoto kubwa katika utoaji huduma ya kinywa na meno kwa ufanisi.

Jengo la kinywa na meno katika hospitali ya wilaya ya Hai limegharimu kiasi cha shilingi milioni 82 hadi kukamilika kwake likitegemewa kuleta mapinduzi makubwa kwenye huduma mbalimbali za kinywa na meno ambazo awalii hazikuweza kufanywa kwenye hospitali hiyo kwa sababu ya kukosa vifaa.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai