• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

"Tumejipanga Kuwahudumia Wananchi wa Wilaya ya Hai kwa Ufanisi": Mhe. Mafuwe

Imetumwa: November 30th, 2020

Mbunge wa Jimbo la Hai Mhe. Saashisha Mafuwe amewahakikishia wananchi katika wilaya hiyo kuwa Serikali imeweka mikakati madhubuti ya kuboresha maisha yao katika kipindi cha miaka mitano ya 2020 hadi 2025.

Akizungumza kwenye kikao na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai mapema leo Jumatatu Novemba 30, 2020 Mafuwe amesema kuwa viongozi na watumishi wa umma wapo kwenye nafasi zao ili kuwatumikia wananchi.

“Wananchi wa Wilaya ya Hai ndiyo mabosi na waajiri wetu. Mimi Mbunge, Mkurugenzi na watumishi wote tunao wajibu wa kuwatumikia wananchi na kuhakikisha tunaboresha maisha yao”

“Sisi tuliopo humu ndiyo wenye jukumu la kujibu matarajio ya wananchi wa Hai ambao wanaonesha Imani kubwa kuwa jimbo hili sasa linaenda kubadilika” Amesema.

Mafuwe amesema kuwa kazi yake ya kwanza ni kushirikiana na halmashauri kuongeza mapato kwa kubuni vyanzo vipya na kuimarisha yanzo vilivyopo akiamini kuwa serikali yenye pesa inaweza kutoa huduma kwa uhakika.

“Tutafute mapato ili tuweze kutoa huduma kwa wananchi kwenye jimbo na wilaya yetu. Serikali yenye fedha inaweza kutoa huduma za elimu, afya, barabara na nyinginezo kwa uhakika na ufanisi zaidi” Amesisitiza Mafuwe

Aidha, Mafuwe amesema atashirikiana kwa karibu na watumishi wa halmashauri kila mmoja kwa eneo lake la ubobezi ili kutoa huduma sahihi na ya kuridhisha kwa wananchi.

Amewataka wataalamu hao wa halmashauri kuwa tayari kutumia taaluma zao kwenye kutekeleza vipaumbele vya kuifanya Wilaya ya Hai kuwa ya uchumi wa kilimo na viwanda.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo amemuhakikishia Mbunge Mafuwe kuwa ofisi yake na idara zote za halmashauri ziko tayari kufanya kazi kwa kushirikiana na mbunge kufanikisha lengo kuu la kuwahudumia wananchi wa jimbo la Hai.

Mbunge wa Jimbo la Hai Mhe. Saashisha Mafuwe amefanya kikao na watumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Hai ikiwa ni sehemu ya kujitambulisha kwao na kuweka mikakati ya kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi katika kuwahudumia wananchi wa jimbo la Hai.



Matangazo

  • TANGAZO LA UKUSANYAJI NA UZOAJI TAKA HAI MJINI September 27, 2023
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA (PSLE) 2023 WILAYA YA HAI November 23, 2023
  • MAJINA YA WALIOITWA USAHILI NAFASI ZA JESHI WILAYA YA HAI September 06, 2023
  • TANGAZO LA UKUSANYAJI NA UZOAJI TAKA HAI MJINI September 27, 2023
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Mhe Kaijage Awataka Watumishi Kufanya Kazi Kwa Bidii

    November 22, 2023
  • Mkalipa Ataka Viongozi Wa Dini Kufundisha Waumini

    November 08, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Sanya Station Washukuru Ulipwaji Wa Fidia

    October 25, 2023
  • Mkurugenzi Dionis Myinga Aishukuru Kambele Kwa Msaada Wa Sementi

    October 23, 2023
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 27 Hai

    Simu: 0272758441

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai