• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Ujenzi Wa Shule Ya Sekondari Kata Ya Mnadani Kuondoa Adha Ya Wanafunzi Kutembea Umbali Mrefu

Imetumwa: March 10th, 2022

Wananchi wa kata ya  Mnadani Wilayani Hai  wameipongeza serikali kwa kutoa fedha shilingi Millioni  470  kwa ajili ya ujenzi wa  shule mpya ya sekondari ya Shirimatunda

Waliyasema hayo wakati wakishiriki kuchimba msingi kwa ajili ya ujenzi wa vyumba  vya madarasa shuleni hapo wakishirikiana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo  ikiwa ni hatua ya kuunga mkono juhudi za serikali, ambapo walisema mpango wa serikali kutoa fedha hizo umelenga kuwawezesha watoto kusoma katika mazingira rafiki.

Diwani wa kata ya Mnadani  Nasib Mndeme aliwapongeza wananchi wa kata hiyo kwa kujitokeza ambapo amewaomba kuendelea na ushirikiano ili kuipeleka haraka shughuli hiyo  ya ujenzi wa vyumba vya madarasa

Mndeme  ameihakikishia serikali kuwa pesa hiyo waliyopatiwa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ataisimamia vizuri ili malengo yaliyokusudiwa yaweze  kukamilika kikamilifu

Kwa upande wake  Magreth Matiliya kutoka kijiji cha  Shirimatunda ,amesema Ukosefu wa shule ya sekondari katika kata hiyo imekuwa changamoto kwa wanafunzi wa kata hiyo hali inayowalazimu wanafunzi kutembea umbali wa kilomita 8 hadi  sekondari ya Mailisita huku wengine wakilazimika kwenda kata ya  Weruweru  kwa ajili ya masomo.

Alex Utaro, ni miongoni mwa wakazi wa kata hiyo  amesema kuwa wanafunzi wote wanaochaguliwa kujiunga na sekondari katika kata hiyo wanalazimika kuondoka saa kumi alfajir kwenda kata jirani ambapo kuna shule ya sekondari jambo ambalo ni hatari kwa usalama wao.


Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Dionis Myinga  alisema halmashauri hiyo imepokea fedha kutoka serikali kuu chini ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa na UVIKO 19 ,ambazo zimelenga kuwezesha wanafunzi wote wa kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo 2022 kujiunga na kidato cha kwanza kwa wakati mmoja,badala ya awamu mbili.

Edmund Rutaraka  ambae pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Hai amesema ujenzi wa shule ya sekondari Shirimatunda umegharimu  nguvu za wananchi na Serikali  ambapo aliwaomba wananchi kuendela kuchangia mali na nguvu zao kwenye miradi ya maendeleo.

Hata hivyo mkuu wa Wilaya hiyo , Juma Irando  aliwaomba wananchi kuwa tayari kuchangia miradi ya maendeleo wakati miradi inapo anzishwa ili kuondoa changamoto zinazo wakabili wananchi  na kuondokana  na kutembea umbali mrefu kufuata  elimu kata ya jirani pamoja na huduma za afya

Kata ya mnadani ina shule moja ya sekondari na Shule  kumi za Msingi ambapo kati ya hizo  sita ni za serikali na nne zinamilikiwa na taasisi za watu binafsi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai