• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Vijana Watakiwa Kugeuza Changamoto za Jamii kuwa Fursa za Kipato

Imetumwa: October 14th, 2020

Vijana wametakiwa kutumia changamoto zilizopo kwenye jamii na kuzitumia kama fursa ya kujinufaisha kiuchumi kwa kutafuta utatuzi wa changamoto hizo.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Vijana Mkoa wa Kilimanjaro Irine Kiata kwenye maadhimisho ya wiki ya vijana na kumbukizi ya Baba wa Taifa katika viwanja vya halmashauri Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.

Ametoa mfano wa changamoto ya uwepo wa taka inaweza kugeuzwa fursa kwa kuanzisha shughuli za kuzoa taka kwa malipo kutoka kwa wananchi watakaofaidi huduma hiyo na kufanya vijana kupata ajira na kujiongezea kipato.

“Vitabu vya maandiko vinatuambia kuwa sisi vijana tuna nguvu; na fahari yetu ni nguvu. Napenda kuwasihi vijana; mwendelee kufanya kazi kwa bidii na kwa kupitia nguvu zetu tutafanikiwa”

“Niombe pia mashirika tunayoshirikiana nayo kuanza kubadili mipango yao katika kuhudumia vijana kwa kuanza kuwapa elimu wanayostahili badala ya kusubiri waharibikiwe na kuanza kushighulikia matokeo. Tuwape vijana elimu ya namna bora ya kufanya mambo yao kwa ufanisi bora zaidi” Ameongeza Kiata.

Aidha Kiata ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Hai kwa kutambua umuhimu wa vijana na kuwapa nafasi ya kushiriki kwenye maadhimisho ya siku yao kwa kuonesha vipawa vyao kwenye ubunifu, Sanaa, biashara na nyingine pamoja na kuwapa nafasi ya kubadilishana uzoefu na kujifunza kutoka kwa vijana wenzao waliofanikiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo ameahidi kusimamia utekelezaji wa kazi za Serikali katika halmashauri yake ikiwemo shughuli za Kitaifa kuadhimishwa kwa wakati wake kama ilivyo kumbukizi ya Kifo cha Mwalimu Nyerere.

Sintoo amesema kuwa halmashauri ya Hai itaendelea kutoa usaidizi kwa vijana ikiwemo kuwapatia mikopo isiyo na riba pamoja na kuwakutanisha na elimu ya ujasiriamali ili waanzishe miradi yenye tija itakayowaongezea kipato na kuweza kutengeneza ajira kwa vijana wengine.

Amesema halmashauri yake inatekeleza hayo ikiwa ni namna ya kumuenzi Baba wa Taifa kwa vitendo katika kupambana na maadui watatu wa ujinga, umasikini na maradhi.

Awali akisoma risala kwa mgeni rasmi; Afisa Vijana Wilaya ya Hai Lucila Chima amesema Serikali kwa upande wake imeweka sera na mipango madhubuti ya kuwaendeleza vijana katika kujiajiri, kuanzisha na kuendeleza viwanda, kudumisha amani, usawa na kuleta maendeleo kwa kutumia rasilimali na fursa zilizopo kwenye maeneo yao.

Chima amewakumbusha vijana wenzake kutumia fursa za mazingira yaliyowekwa na Serikali ili kujitengenezea shughuli za kuwaingizia kipato na kuwasaidia kujikwamua na umasikini ikiwa ni pamoja na kutengeneza ajira kwa vijana wenzao katika sekta za kilimo, usafirishaji, Sanaa na ubunifu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai