• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Wanafunzi Watatu Mbaroni Wakituhumiwa Kuchoma Bweni

Imetumwa: October 17th, 2020

Wanafunzi watatu wanaosoma masomo ya Dini Katika Chuo kinachotoa mafunzo ya Quran na hadithi za Mtume cha  Othuman Binhassan kilicho chini ya Msikiti wa Othman Bomang’ombe Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wakituhumiwa kuchoma moto bwalo la chakula linalotumiwa na wanafuzi wa chuo hicho.

Tukio la kuchomwa moto bwalo hilo limetokea Jumapili ya tarehe 11 Octoba 2020 wakati waumini wa msikiti huo wakiendelea na Swala ya adhuhuri ambapo kufuatia tukio hilo mkuu wa wilaya ya Hai ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya Lengai Ole Sabaya amefika msikitini hapo kukagua athari na kupata taarifa ya tukio hilo.

Sabaya amesema kuwa tayari Jeshi la Polisi wilayani humo linawashikilia wanafunzi watatu ambao wamekiri kuhusika na tukio hilo huku akilipongeza jeshi la polisi kwa jitihada walizofanya kwa muda mfupi za kufanikisha kuwakamata na kulitaka jeshi hilo kuendelea na uchunguzi ili kubaini sababu za tukio hilo.

“OCD mimi nakupongeza sana wewe na vijana wako kwa kazi mliyoifanya ya kuhakikisha kwamba angalau tumetatua kitendawili cha nani amechoma, hili ni tukio letu la kwanza kwenye wilaya ya Hai na tulikubaliana kwamba kwenye wilaya hii matukio ya namna hiyo hayatatokea”. Amesema Sabaya.

“Hapa tumepata watu watatu ambao wamethibitika wamechoma moto jengo hilo, kwa hiyo muendelee kuwahoji vizuri wawaambie kama kuna wengine na waseme wanafanya project ya nani na walitaka kuwauwa wangapi ili tufikishe hitimisho hii ajenda mpya yakuchoma maeneo na taasisi mbalimbali”. Ameongeza Sabaya.

Aidha Sabaya ameuomba uongozi wa msikiti na chuo hicho kuhakikisha kuwa unaendeleza uhusiano mzuri baina yao na serikali kwani kwa kupitia ushirikiano wa katibu ni rahisi kubadilishana taarifa na kuweza kuzuia vitendo vya uhalifu kabla havijatokea.

Awali akisimulia tukio hilo Msimamizi Mkuu wa chuo hicho na imamu wa msikiti huo Abdala Juma amesema kuwa kabla ya tukio la moto kulitokea upotevu wa simu za wanafuzi 68 ambazo ziliibiwa na wanafuzi hao watatu na kwenda kuzificha kwenye dari la msikiti ambapo amesema kuwa walipowahoji wanafunzi hao walisema kuwa waliamua kuchoma jengo hilo moto ili chuo kifungiwe na wao wapate fursa yakutoroka na simu hizo.

“Tuna utaratibu wanafunzi wote wakifika simu zao tunazichukua na kuziweka kwenye chumba cha kiongozi, watuhumiwa hao walivizia tukiwa msikitini wakaiba zile simu zote wakazificha na baada ya hapo tukafanya uchunguzi wakahisi tutawakamata.”

“Baada ya tukio tuliwahoji wakasema waliamua kuwasha moto ili chuo kifungwe na kikishafungwa wapate fursa ya kuchukua zile simu waondoke nazo kutoka mahali walipozificha juu ya dari ndani ya msikiti”. Amesema Imamu Abdala Juma.

Kuhusu madhara amesema kuwa moto huo umeteketeza magodoro 8, mabegi sita na nguo chache za wanafuzi huku vitu vingine vikiokolewa.

Hivi karibuni kumekuwa na mfululizo wa matukio ya kuungua kwa moto mabweni katika shule mbalimbali hapa nchini ambapo mpaka hivi sasa jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi katika matukio hayo ili kubaini chanzo chake.


Matangazo

  • TANGAZO LA UKUSANYAJI NA UZOAJI TAKA HAI MJINI September 27, 2023
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA (PSLE) 2023 WILAYA YA HAI November 23, 2023
  • MAJINA YA WALIOITWA USAHILI NAFASI ZA JESHI WILAYA YA HAI September 06, 2023
  • TANGAZO LA UKUSANYAJI NA UZOAJI TAKA HAI MJINI September 27, 2023
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Mhe Kaijage Awataka Watumishi Kufanya Kazi Kwa Bidii

    November 22, 2023
  • Mkalipa Ataka Viongozi Wa Dini Kufundisha Waumini

    November 08, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Sanya Station Washukuru Ulipwaji Wa Fidia

    October 25, 2023
  • Mkurugenzi Dionis Myinga Aishukuru Kambele Kwa Msaada Wa Sementi

    October 23, 2023
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 27 Hai

    Simu: 0272758441

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai