• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Wananchi Wa Kijiji Cha Kware Kata Ya Masama Kusini Waishuru Serikali

Imetumwa: June 27th, 2025

Wananchi wa kijiji cha Kware wilayani Hai mkoani Kilimanjaro wameishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha mbalimbali kwaajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kijiji hicho.


Akitoa taarifa ya mapokezi ya fedha kiasi cha 49,000,000/= (Milioni arobaini na tisa laki nane) fedha ambazo zitatumika katika zahati ya kware, afisa mtendaji wa kijiji hicho Edwine Lamtey amesema kuwa fedha hiyo ni kwaajili ya mradi wa Usambazaji endelevu wa maji vijijini na usafi wa mazingira (Sustainable rural water supply and sanitation.)


Aidha pia amesema kuwa fedha hiyo itatumika kwaajili ya kuboresha miundo mbinu ya maji, vyoo, kichomea taka, shimo la kutupia kondo la nyuma pamoja na shimo la kutupa majivu.


"Tumepokea fedha hizi, kazi yangu mimi kama msimamizi wa hii miradi ni kuhakikisha inatekelezwa kama ilivyokusudiwa na serikali pamoja na kuhakikisha thamani ya fedha katika mradi ionekane na pia niwatake watumishi pamoja na wale mtakaoingia katika hizi kamati hii ni fedha ya serikali itatumika kwa malengo mahususi tu" Alisema Edwine Lamtey.


Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho mwenyekiti wa kijiji cha Kware Sabastian Kimaro amesema kuwa mbali na ujio wa fedha hiyo, hivi karibuni kijiji kilipokea milioni kumi kwaajili ya ununuzi wa madawati, Milion 3 fedha ya mfuko wa jimbo kwaajili ya ujenzi wa jiko ambao uko mbioni kukamilika.


"Pamoja na hizi nilizozitaja Kware sasa tumeamka na tunapambana kupata maendeleo ambayo hapo awali tuliyapoteza, Leo nini ni mashuhuda tunaenda kupaua ofisi yetu mpya na tayari vifaa vya upauzi tunavyo ambavyo ni wanachi wa kware wamejitoa na siri kubwa ni ushirikiano wa viongozi wa kijiji na wananchi" Alisema Mwenyekiti Kimaro.


Nae Sabrina Lema ambaye ni mwananchi wa kitongoji cha Boma Kati kilichopo kijijini hapo amesema kuwa kwa muda mfupi kumekuwa na maendeleo makubwa ikiwa ni muunganiko mzuri na ushirikiano kati ya wananchi, serikali ya kijiji pamoja na viongozi wa juu.


Katika mkutano huo pia wananchi wa kijiji hicho walipewa elimu ya urasimishaji wa ardhi ikiwa ni njia ya kuiongezea ardhi thamani pamoja na kupunguza migogoro ya ardhi, zoezi ambalo litaanza hivi karibuni.


Kijiji cha Kware ni miongoni mwa vijiji vinne vilivyopo katika kata ya Masama Kusini ambapo kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi kijiji hicho kina idadi ya watu 1750 huku shughuli kubwa zikiwa ni kilimo, ufugaji pamoja na biashara.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA UDEREVA, MWANDISHI MWENDESHA OFISI, MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU NA MHUDUMU WA JIKONI June 02, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Wananchi Wa Kijiji Cha Kware Kata Ya Masama Kusini Waishuru Serikali

    June 27, 2025
  • Serikali Kuboresha Soko La Parachichi

    June 11, 2025
  • Ng'ombe Elfu 88 Kupata Chanjo Ya Mapafu Wilayani Hai

    June 12, 2025
  • Mashirika Yasiyo Ya Kiserikali Yametakiwa Kushirikiana

    June 10, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai