• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Wananchi Wametakiwa Kupanda na Kutunza Miti

Imetumwa: April 13th, 2021


Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Hai wametakiwa kujenga mazoea ya kupanda miti kila inapofika kipindi cha mvua ili kuimarisha mazingira yanayowazunguka.

Wito huo umetolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Hai Upendo Wella wakati akizindua wiki ya upandaji miti katika wilaya hiyo.

Wella amesema ili kuwa na mazingira rafiki kwa ajili ya binadamu na viumbe vingine ipo haja ya wananchi kupanda miti kwa wingi kwani uwepo wa mitiya kutosha unasaidia kuboresha maisha ya viumbe hai.

Ametumia uzinduzi huo kuwakumbusha wananchi wa maeneo ya Bomang’ombe hali ilivyokuwa miaka minne iliyopita na kukiri kuwa mazingira yameimarika kwa kiasi kikubwa kutokana na juhudi zinazochukuliwa za kupanda miti na kutunza mazingira.

Aidha Wella amewahamasisha wananchi kuanza kujihusisha na kilimo cha zao la korosho ambalo limetambulishwa katika Wilaya ya Hai baada ya utafiti kubaini zao hilo kustawi maeneo ya ukanda wa chini wa wilaya hiyo.

“Niwahimize kuanza kilimo cha korosho kwa sababu ni moja ya mazao ya kimkakati yanayopigiwa chapuo na Serikali lakini pia ni chanzo kikubwa na cha uhakika cha kipato kwa mtu mmojammoja na hatimaye kwa Taifa zima” Amesema Wella.

Kwa upande wake Afisa Maliasili Wilaya ya Hai Mbayani Mollel amesema kuwa jumla ya miti 3000 imepandwa siku ya uzinduzi katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, Kituo cha Polisi Wilaya pamoja na Hospitali ya wilaya ya Hai na kwamba zoezi la upandaji litaendelea kwenye taasisi za Serikali ikiwemo vituo vya huduma za afya, shule na ofisi za Umma.

Mollel amesema kwamba Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imepanga kuotesha miti milioni moja na laki tano kila mwaka ili kuimarisha mazingira, kutokomeza hali ya jangwa na kuifanya dunia makazi salama kwa wanadamu na viumbe wengine.

Naye Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la VOEWOFO Asifiwe James ambaye shirika lake ni mdau wa masuala ya kijamii amesema wataendelea kushirikiana na Serikali katika masuala yote yanayohusu ustawi wa wananchi ikiwemo kuotesha na kutunza miti kwani kwa kufanya hivyo wanachangia kuboresha maisha ya wananchi.

Kila mwaka maadhimisho ya wiki ya upandaji miti hufanyika kwa kuotesha miti ya matunda na kivuli kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo taasisi za umma na kuendelea kuwahamasisha wananchi kupanda na kutunza miti kwenye maeneo ya makazi na biashara.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai