• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Washauriwa Kupanda Miti Kupambana Changamoto za Mazingira

Imetumwa: November 20th, 2020

Katika msimu huu wa mvua za vuli ambazo zinaendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali, wananchi wilayani Hai wameshauriwa kuendelea kupanda miti katika maeneo yao ili kuepukana na changamoto za kimazingira zinazoikabili dunia kwa sasa.

Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na Afisa misitu katika Wilaya ya Hai Badi Hatibu aliposhiriki zoezi la kupanda miti katika tindiga la Boloti na kusema kuwa bado jitihada kubwa zinahitajika kwa wananchi kutambua umuhimu wa upandaji miti ambao utarejesha uoto wa asili ulioharibiwa na shughuli za kibinadamu.

Hatibu amesema kuwa shughuli za kibinadamu katika maeneo yaliyohifadhiwa ikiwemo eneo oevu la Boloti bado zimeendelea kuathiri uoto wa asili na kuleta changamoto kubwa za uhifadhi wa mazingira huku akidai kuwa uharibifu huo umekuwa na madhara ya moja kwa moja kadiri siku zinavyosonga.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika la Floresta Tanzania ambalo ni moja ya wadau wa mazingira mkoa wa Kilimanjaro Richard Mhina amesema kuwa wananchi wanapaswa kuona umuhimu wa uhifadhi wa mazingira kwa faida yao binafsi.

Mhina amesikitishwa na kitendo cha uharibifu unaoendelea katika eneo oevu la tindiga la Boloti lililohifadhiwa ambapo amesema kuwa wameshirikiana mara nyingi na ofisi ya misitu wilaya kupanda miti katika eneo hilo huku changamoto kubwa ikiwa ni uhifadhi wa miti hiyo ambapo mifugo wamekuwa wakiingia na kuiharibu kila wakati.

Kwa upande wake Kundankira Kimaro mkazi wa Kijiji cha Kware ameziomba serikali za vijiji vinavyozunguka eneo hilo kuona kuwa inao wajibu wa kuchukua hatua kali ili kulinda eneo ambalo yeye ameeleza kuwa endapo litatumiwa vyema litakuwa na tija kwa jamii kubwa.

Ikumbukwe kuwa eneo la Boloti lilitengwa na serikali kama eneo oevu japo kwa sasa linakumbwa na changamoto lukuki ikiwemo kuendelea kwa shughuli za kibinadamu ndani ya eneo hilo huku mamlaka husika zikifumbia macho bila kuchukua hatua zozote.

Kwa mujibu pia wa taarifa kutoka ofisi ya misitu wilaya zinaonesha kuwa ni zaidi ya mara nne wanapanda miti katika eneo hilo bila mafanikio katika uhifadhi na kwa wiki hii pekee miti zaidi ya elfu nane imepandwa kwa mara nyingine na swali kubwa likiwa ni Je endapo miti hiyo italindwa ama la.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai