• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Watanzania Watakiwa Kuiunga Mkono Serikali Kuleta Maendeleo

Imetumwa: May 23rd, 2018

Watanzania wametakiwa kuiunga mkono serikali katika juhudi zake za kuwaletea maendeleo kwenye maeneo yao kwa kushiriki kulipa kodi mbalimbali zilizowekwa kisheria huku wakitambua kuwa kodi ni msingi wa maendeleo ya nchi hasa kwa wakati huu ambapo nchi inajizatiti kuelekea uchumi wa wa kati kwa kuimarisha viwanda.

Wito huo umetolewa mapema leo Mei 23  na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Dk. Hasani Abass kwenye mahojiano na kituo cha Redio Boma Hai cha Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro alipokuwa kwenye ziara ya kikazi ya kuwatembelea maafisa Habari na Mawasiliano wa Sekretarieti za mikoa na mamlaka za serikali za mitaa.

Amesema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Magufuli imejizatiti kuwahudumia na kuwatumikia wananchi wake kwa kutatua changamoto mbalimbali za wananchi katika maswala ya maji, umeme pamoja na kufufua viwanda vidogo na vikubwa kwa lengo kuu la kuboresha maisha ya Mtanzania mmojammoja nan chi nzima kwa ujumla.

“Niwaombe wananchi waendelee kuiunga mkono serikali yao kuanzia viongozi waliopo kwenye ngazi ya wilaya yaani Mkuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Wabunge, Madiwani nikiamini kuwa viongozi wote hawa wana dhamira ileile ya Mhe. Rais ya kuona mtanzania anaondokana na kero ambazo hazina msingi wala hazina sababu ya kuwepo lakini pia viongozi waliopo niwaase waendelee kutekeleza kazi zao kwa kasi kama ambavyo Mhe. Rais anataka ili wananchi waweze kuona matokeo chanya”. Ameongeza Dkt. Abbas.

Aidha Dkt. Abbas amewataka wananchi kufuatilia kwa karibu utendaji wa serikali ya awamu ya tano na kujionea hatua zinazopigwa katika kuleta maendeleo ya nchi kwani kwenye kila sekta kuna kazi kubwa ya kimageuzi inafanyika huku akitolea mfano sekta ya nishati inayoboreshwa kwa utekelezaji wa miradi ya Kinyerezi I ambayo upanuzi wake ukikamilika utazalisha megawati za umeme 185; mradi wa Kinyerezi II utakaozalisha megawati 240 umeshazinduliwa pamoja na mradi mkubwa wa Stigler’s Gorge ambao ni mradi wa kihistoria utakaozalisha megawati 2100 za umeme ukiwa kwenye hatua ya uchambuzi baada ya kutangaza zabuni.

Pamoja na miradi mingine, Dkt. Abbas amezungumzia utekelezaji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa reli ya kisasa itakayounganisha Tanzania na nchi jirani ya Rwanda ambayo itaanzia Daresalam huku akibainisha kuwa treni hizo zitaendeshwa kwa umeme huku serikali ikipiga hatua nyingine kubwa ya kutangaza zabuni ya kuleta mabehewa na vichwa vya treni 1590 ambapo kati yake mabehewa 1560 yatakuwa ya kubeba mizigo ya aina mbalimbali na yaliyobaki yatakuwa ya kubeba abiria.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO)  Paschal Shelutete amewakumbusha  maafisa habari wa  Halmashauri jukumu lao kuu la kuwahabarisha wananchi kuhusu maswala ya maendeleo na kuwataka wasiwe kikwazo cha utoaji taarifa kwa wananchi  bali wao wawe chachu ya kufanikisha taarifa kuwafikia wananchi kuhusiana na utekelezaji wa kazi za serikali katika maeneo yao kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wametekeleza vizuri jukumu lao la kumsaidia Mhe. Rais katika juhudi za kuleta maendeleo nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai