• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Watumishi Wampongeza DC Ushiriki Kuboresha Huduma za Afya

Imetumwa: February 12th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya amewashukuru kwa zawadi aliyopewa na watumishi wa Idara ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Hai kwa kutambua mchango wake katika kazi wanazofanya huku akisisitiza kuwa lengo kuu ni kuwapunguzia wananchi changamoto wanazokutana nazo.

Sabaya amesema ni jambo jema kwa kutambua mchango wa mtu kwenye jamii kwa sababu inatia moyo kwa anayetambuliwa lakini pia inaamsha ari ya kujituma na kufanya kazi kwa bidii akiamini kuwa utamaduni huo utasaidia kuboresha huduma zinazotolewa kwa wananchi katika ngazi zote.

Sabaya ameshiriki kikamilifu katika kuibua wazo la kujenga kituo cha afya cha kisasa kwenye ukanda wa tambarare wa wilaya ya Hai na kuvishirikisha vyama vya ushirika vilivyopo kwenye wilaya hiyo hatimaye kufanikiwa kupatikana fedha kiasi cha shilingi milioni 38 zinazotumika kujenga kituo cha afya cha Longoi.

Aidha Sabaya ametoa wazo la kuanzishwa au kuimarishwa huduma kadhaa katika vituo vya kutolea huduma za afya ikiwemo hospitali ya wilaya ya Hai. Mojawapo wa huduma hizo ikiwa ni kitengo cha huduma za kinywa na meno iliyozinduliwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. David Silinde.

Imefahamika kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo amekuwa mstari wa mbele katika kuimarisha utendaji kazi wa Idara ya Afya kupitia hospitali ya wilaya pamoja na vituo vya kutolea huduma kwenye wilaya hiyo hadi kupelekea watumishi hao wakiongozwa na Mganga Mkuu wa halmashauri hiyo Dkt. Irene Haule kukabidhi zawadi hiyo.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Dkt. Irine Haule amesema kuwa Mkuu wa wilaya huyo amekuwa mara kwa mara akitoa ushauri wa namna bora ya kutekeleza kazi mbalimbali zinazohusu huduma za afya kwenye wilaya hiyo ikiwemo kutatua migogoro mbalimbali inayojitokeza.

“Mara kwa mara Mkuu wa Wilaya amekuwa msaada kwetu katika kutekeleza kazi zetu hasa pale tunapokutana na changamoto za kimaamuzi; mfano wa karibu ni ushiriki wake wakati wa kuandaa mpango wa bajeti ya afya kwa mwaka wa fedha 2021/2022” Amesema Dkt. Haule.

Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo wakiwemo Katibu Tawala Upendo Wella na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Yohana Sintoo wamekuwa chachu ya maendeleo katika halmashauri hiyo katika sekta mbalimbali kama afya, elimu, maji, nishati na nyingine katika kuboresha maisha ya wananchi katika wilaya hiyo.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Ujenzi Wa Bweni La Shule Ya Machame Kukamilika Kabla Ya June 19

    May 29, 2025
  • Vijana Wasauriwa Kutumia Fursa

    May 27, 2025
  • Wafanyabiashara Wa St Stend Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Wafanyabiashara Wa Send Wasikilizwa

    May 22, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai