• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Wilaya ya Hai Kujenga Kituo cha Afya kwa Mapato ya Ndani

Imetumwa: December 13th, 2019

Zaidi ya wanachi 27,000 wa kata za Weruweru, Mnadani na Masama Rundugai wanatarajia kunufaika na huduma ya afya kutoka katika kituo cha afya kinachojengwa katika kijiji cha Longoi kata ya Weruweru kinachokadiriwa kugharimu zaidi ya milioni 500 kutoka katika mapato ya ndani.

Akizungumza katika uzinduzi wa ujenzi wa kituo hicho  uliofanyika leo katika Kijiji cha Longoi Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya amesema ujenzi wa kituo hicho ni maelekezo ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Magufuli kwenda kwa wasaidizi wake lengo likiwa ni kuwaondolea kero wananchi maeno ambao hawana huduma hiyo tangu nchi ipate uhuru.

Amesema fedha za awali za ujenzi wa kituo hicho kiasi cha shilingi 388,552,415, kimetokana na michango ya vyama vya ushirika wilayani humu na kwamba kukamilika kwa ujenzi huu utakipa heshima ushirika ambao kwa mingi mingi sasa umekuwa ukituhumiwa kwa ubadhilifu wa fedha.

“milioni 388 itamaliza jengo la maabara ya upimaji, jengo la wagonjwa wa nje na jengo la mama na mtoto ,na akina mama waliokuwa wanatoka hapa wanavuka kale kadaraja kareli usiku wa manane wanapitia shirimgungani hadi mijongweni hadi shirimatunda hawatakwenda tena huduma zenu sasa zimeletwa hapa”alisema Sabaya.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa Kituo hicho Mganga mkuu wa wilaya Dr.Irene Haule amesema wazo la ujenzi wa kituo hicho cha Afya lilitolewa na mkuu huyo wa wilaya kwakushirikiana na kamati ya ulinzi na Usalama  na kwamba kitawasadia wananchi wa kata hizo ambao baadhi yao wamekuwa wakitembea umbali zaidi ya km 20 kufuata huduma za Afya katika katika hospitali ya Wilaya.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo ameahidi kuzisimamia kikamilifu fedha hizo na kuhakikisha kuwa ujenzi wa kituo hicho unakamilika kwa wakati huku akiwataka wananchi wa eneo hilo kutoiba wala kuaribu mioundo mbinu ya mradi huo na kwamba yeyote atakaebainika atachukuliwa hatua kisheria.

Nao baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Longoi; Mwajuma Athumani na Miraji Athumani wameishukuru serikali kwa kuona umuhimu wa kuwapelekea kituo hicho cha afya kwani wamekuwa wakitumia gharama kubwa kufuata huduma za afya na wakati mwingine wamekuwa wakipoteza ndugu zao kutokana na huduma hizo kuwa mbali.

Wilaya ya Hai ina jumla ya vituo vya kutolea huduma 60 ambavyo kati ya hivyo vituo 2 Ni hospitali ya wilaya na hospitali teule ya Machame ambapo kati ya hivyo vimo vituo vya binafsi na vya mashirika ya dini.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai