• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Accounts and Finance
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Wilaya ya Hai Yajizatiti Kuboresha Lishe

Imetumwa: September 16th, 2019

HALMASHAURI ya wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro inatazamia kutumia zaidi ya shilingi milioni 30 kwa ajili ya kuboresha utendaji wa kazi ya kusimamia shughuli za lishe ngazi ya jamii.

Fedha hizo ambazo zimetengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2019 /2020 zitasaidia ufuatiliaji na utoaji wa elimu ya lishe  ili kuhakikisha kuwa jamii nzima ya wilaya ya Hai inakuwa na afya njema na kuondokana na magonjwa yanayosabaishwa na ukosefu wa lishe.

Akizungumza  na watendaji wa kata na vijiji katika kikao kazi cha kuweka mkataba wa utendaji kazi na usimamizi wa shughuli za lishe ngazi ya jamii wilayani Hai, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Yohana Sintoo , amesema  kuwa halmashauri imejipanga kuhakikisha kuwa inatoa elimu ya kutosha kwenye jamii kwa kupitia viongozi waliopo kwenye maeneo yao.

Amefafanua kuwa zoezi la utoaji wa elimu kwa ajili ya lishe , litafanyika kwa ngazi zote lengo ikiwa ni kufikia wananchi kuanzia nagzi za vitongoji hali ambayo itasaidia kuondoa utapiamlo unaosababishwa na upungufu wa virutubisho au kuwa na wingi wa virubisho kupita kiasi mwilini.

Kwa upande wake Afisa Lishe wilaya ya Hai, Silvania Ignace amesma kuwa lengo la mpango huu ni kuhakikisha jamii kupitia viongozi wao kwa pamoja wanashiriki ipasavyo katika kupanga na kutekeleza kufuatilia maendeleo ya kazi za lishe na malezi ya watoto.

"Viongozi wa kata hakikisheni kuwa wadau wa lishe wote waliopo kwenye kata wanatambulika na wanawasilisha taarifa zao kwenye kamati za kata pamoja na kuhakisha kuwa wanafanikisha hali lishe na kupunguza athari za utapiamlo kwenye jamii”amesema

“Naombeni sana katika vikao vyenu kwenye vijiji kuhakikisha kuwa mnatoa taarifa za lishe kila robo ya mwaka ili kuweza kujua   mafanikio yanayopatikana  katika zoezi hili ” amesema Ignace.

“Pia napenda kuwakumbushia wahudumu wa afya ya jamii wahakikishe wanatembelea kaya na kutoa elimu ya lishe, Afya uchangamshi maji na usafi wa mazingira na vilevile kila kijiji kushirikiana na vituo vya kutolea huduma za afya katika zoezi la utoaji wa nyongeza ya vitamin kwa watoto wenye umri wa miezi 6-59” amefafanua afisa huyo.



Awali akifungua kikao hicho kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, Katibu  Tawala wa wilaya, Upendo  Wella amewataka watendaji hao kuhakisha wanatoa ushirikiano katika utekelezaji wa mkataba waliosaini ili kuhakikisha kuwa jamii inakuwa na afya bora kwa kuzingatia mambo yaliyoorodheshwa  kwenye mkataba.

 “Watendaji wa vijiji na kata wamehusishwa moja kwa moja wakawe wajumbe au wasimamizi kuhakikisha jamii ambazo wanaziongoza zinakuwa na lishe bora” amesema Wella.

Wilaya ya Hai kwa sasa ina asilimia 29 ya watoto wanaokabiliwa na tatizo la udumavu wa lishe jambo ambalo wameliwekea mikakati ya kuondoa tatizo hilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA YA UDEREVA March 28, 2025
  • TANGAZO LA MKOPO KWA WATUMISHI December 20, 2024
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA HAI 2024 December 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA October 29, 2024
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Shule Ya Msingi Nguzo Nne Yashika Nafasi Ya Pili Kwa Usafi

    April 09, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Wananchi Wa Hai Wapo Tayari Kwa Uchuguzi

    April 05, 2025
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ameongeza Anna Boniface

    March 24, 2025
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai

    Simu: 0754553560

    Simu ya Mkononi: 0754553560

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai